Klabu ya Yanga imeweka wazi msimamo wake wa kutowatambua wasimamizi wa mshambuliaji Clement Mzize kwani hawana sifa kwa mujibu wa kanuni
Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Yanga Ali Kamwe amesema kwa mujibu wa kanuni ya 57 ya ligi kuu 2025/26, mwakilishi yeyote wa mchezaji wa ligi kuu anapaswa kuwa na leseni ya FIFA
Kamwe amewataka wale wanaotaka ufafanuzi kutoka upande wa klabu juu sakata la usajili wa mshambuliaji huyo wajiridhishe kama hao wanaojitambulisha kuwa wakala wake wana leseni kwa mujibu wa kanuni?
Hivi karibuni Yanga ilifungua majadiliano na Mzize ambayo inaelezwa yamezaa matunda baada ya mchezaji huyo kukubali kubakia ndani ya Yanga
Yanga imempa Mzize ofa nono iliyoambatana na ongezeko la mshahara na kumpa gari jipya na hivyo amekubali kuendelea kusalia Yanga
Usikose kutazama mechi zote za LIGI KUU TANZANIA BARA, MECHI ZA ULAYA, MASHINDANO YA CAF LIVE bure kupitia Simu yako download App yetu mapema itakayokuwezesha kuzitazama mechi hizi live bure pia ndani ya App yetu utaweza kutazama chanel za Azam tv na Dstv bure bonyeza HAPA au HAPA kudownload app kumbuka app bado hatujaiweka playstore hivo utaidownload kama Apk ikileta neno harmful usiogope.

Post a Comment