TAABU IKO PALE PALE YANGA WAMALIZA ISHU YA MZIZE KIBABE


 Klabu ya Yanga SC iko mbioni kumbakisha mshambuliaji wake chipukizi Clement Mzize licha ya kuvutwa na ofa kadhaa kutoka ndani na nje ya nchi, imefahamika

Taarifa kutoka Makao Makuu ya klabu zimedokeza uongozi umefanikiwa kumshawishi Mzize kwa kumpa mkataba mpya utakaomfanya kusalia Jangwani hadi mwaka 2028.

Awali Mzize alikuwa na mkataba wa miaka miwili, lakini kwa sasa ameongezewa mwaka mmoja zaidi, pamoja na kupewa nyongeza ya mshahara na gari jipya.

Klabu ya Esperance ya Tunisia iliripotiwa kuwasilisha ofa ya dola milioni moja kwa ajili ya kumnasa mshambuliaji huyo, ambaye alifunga mabao mawili katika michuano ya CHAN. Hata hivyo, Yanga iliweka kipaumnbele cha kumshawishi ili abaki.

Mara kadhaa Rais wa Yanga, Injinia Hersi Said, amesema sera ya klabu ni kuhakikisha kwanza nyota muhimu wanabaki, na pale tu inaposhindikana ndipo hatua ya kuwauza hufuatwa.

Yanga imeweka malengo makubwa kwa msimu ujao, ikiwemo kutetea mataji yake yote ya ndani pamoja na kufanya vizuri zaidi kwenye michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Baada ya kumuuza Stephane Aziz Ki, klabu hiyo haikuwa tayari kupoteza mchezaji mwingine muhimu, hivyo kuhakikisha Mzize anasalia kuwa sehemu ya kikosi cha Wananchi msimu ujao.

Usikose kuitazama mechi za michuano ya CHAN na LIGI KUU TANZANIA BARA, MECHI ZA ULAYA LIVE bure kupitia Simu yako download App yetu mapema itakayokuwezesha kuzitazama mechi hizi live bure pia ndani ya App yetu utaweza kutazama chanel za Azam tv na Dstv bure bonyeza HAPA au HAPA kudownload app kumbuka app bado hatujaiweka playstore hivo utaidownload kama Apk ikileta neno harmful usiogope.

0 Comments

Post a Comment

Post a Comment (0)

Previous Post Next Post