Kila mara nilipoingia kwenye uhusiano, nilikuwa na matumaini makubwa kwamba huenda huu ndio ungekuwa wa mwisho. Nilijitahidi kuwa mpenzi mwaminifu, mwenye kujali na kuonyesha mapenzi ya kweli. Lakini mara zote mwisho ulikuwa uleule kuachwa bila maelezo ya maana.
Wakati mwingine nilipigwa kikumbo kwa maneno mepesi kama, “Wewe ni mtu mzuri sana, lakini sidhani kama tutafaa.” Wakati mwingine walikuwa wanatoweka ghafla, wakikata mawasiliano bila huruma. Nilianza kujiuliza kama tatizo lilikuwa mimi.
Kila mara nilipoona rafiki au ndugu akiposti pete ya uchumba kwenye mitandao ya kijamii, moyo wangu ulijaa huzuni. Nilijiuliza kwa nini bahati hiyo haikuniangukia. Hata nilijaribu kubadilika mara kadhaa kufanya mabadiliko ya muonekano wangu, kuvaa vizuri zaidi, hata kujipeleka kwa mafunzo ya kujengea kujiamini.
Lakini bado matokeo hayakuwa tofauti. Nilihisi kama nilikuwa nimezuiliwa na nguvu isiyoonekana, nguvu iliyonifanya nisifike popote katika mapenzi. Soma zaidi hapa

Post a Comment