Mechi ya ligi ya Mabingwa kati ya Gaborone United vs Simba ni September 20


 Msimu huu kabla ya mikiki mikiki ya ligi kuu, itaanza kampeni ya michuano ya ligi ya mabingwa (CAF CL) hatua ya awali ambapo mechi za mkondo wa kwanza zitaanza kupigwa Septemba 19

Simba itaanzia ugenini dhidi ya mabingwa wa Ligi Kuu ya Botswana, Gaborone United mchezo wa mkondo wa kwanza ukipangwa kupigwa Septemba 20

Mechi ya marudiano itapigwa wiki moja baadae katika uwanja wa Benjamin Mkapa

Ni ratiba ambayo imekaa kimtego kwani Septemba 16 Simba inakabiliwa na mchezo wa Ngao ya Jamii dhidi ya Yanga ambapo baada ya mchezo huo italazimika kusafiri kuelekea Botswana

Zipo taarifa kuwa TFF inaweza kufanya mabadiliko ya ratiba ya mchezo huo wa Ngao ya Jamii ili kuzipata nafasi klabu za Simba na Yanga kujiandaa na mechi zao za hatua ya awali ligi ya mabingwa

Yanga ina ahueni kidogo kwa sababu wao watacheza Septemba 21 nchini Angola

Usikose kutazama mechi zote za LIGI KUU TANZANIA BARA, MECHI ZA ULAYA, MASHINDANO YA CAF LIVE bure kupitia Simu yako download App yetu mapema itakayokuwezesha kuzitazama mechi hizi live bure pia ndani ya App yetu utaweza kutazama chanel za Azam tv na Dstv bure bonyeza HAPA au HAPA kudownload app kumbuka app bado hatujaiweka playstore hivo utaidownload kama Apk ikileta neno harmful usiogope.

0 Comments

Post a Comment

Post a Comment (0)

Previous Post Next Post