Jamaa Afichua Anaishi Na Bibi Wake Kwa Siri Ndani Ya Tanki Baada Ya Kukimbia Familia


Wakaazi wa eneo la Igoma mjini Mwanza walipigwa na butwaa Jumanne, Julai 29, 2025, baada ya kufichuka kwamba mwanaume mmoja amekuwa akiishi ndani ya tanki la maji kwa zaidi ya miezi mitano pamoja na mke wake wa pili aliyemwoa kwa siri.

Tukio hilo lilizua gumzo mitaani baada ya majirani kuanza kulalamika kuhusu sauti za ajabu zinazotoka ndani ya tanki hilo hasa wakati wa usiku. Baada ya uchunguzi wa karibu kufanywa na viongozi wa mtaa, walibaini kuwa mwanaume huyo aliyefahamika kwa jina la Paulo M., alikuwa amehamisha maisha yake yote ndani ya tanki la plastiki lililowekwa nyuma ya nyumba ya mama yake mzazi.

Kwa mujibu wa mashuhuda, Paulo aliingia katika mgogoro mkali na familia yake alipowasilisha ombi la kuoa mwanamke kutoka eneo la mbali ambaye familia haikumpenda. “Walimuambia huyo mwanamke ni mchawi, na hawatakubali awe sehemu ya familia yao. Paulo hakusikia,” alisema jirani mmoja kwa masharti ya kutotajwa. Soma zaidi hapa 

0 Comments

Post a Comment

Post a Comment (0)

Previous Post Next Post