TETESI Za Usajili Ligi Kuu Tanzania Bara 2024/2025 - EDUSPORTSTZ

Latest

TETESI Za Usajili Ligi Kuu Tanzania Bara 2024/2025

Klabu za Dodoma Jiji, Mashujaa na JKT Tanzania zinapigana vikumbo kuiwania saini ya Nassoro Kapama ambaye amemaliza mkataba wake wa miezi sita na Mtibwa Sugar iliyoshuka daraja.

Juma Nyangi Mtibwa Sugar

Juma Nyangi Mtibwa Sugar

Klabu za Kagera Sugar, KMC FC, Coastal Union na Dodoma Jiji, zimeonyesha nia ya kuhitaji saini ya kiungo wa Mtibwa Sugar iliyoshuka daraja, Juma Nyangi.

Andy Bikoko Tabora United

Andy Bikoko Tabora United

Klabu za Singida Fountain Gate, Pamba Jiji na Singida Black Stars zimeingia Katika vita ya kuwania saini ya beki wa Tabora United, Andy Bikoko raia wa DR Congo.

Anita Adongo Alliance Girls

Anita Adongo Alliance Girls

Klabu za Simba Queens na Yanga Princess zimeingia kwenye vita ya kumuwinda beki wa kati wa Alliance Girls, Anita Adongo ambaye anamaliza mkataba mwishoni mwa msimu huu.

Nelly Kache Alliance Girls

Nelly Kache Alliance Girls

Klabu ya Ceasiaa Queens inatajwa kuwa miongoni mwa timu zinazohitaji huduma ya Kiungo wa Alliance Girls, Nelly Kache.

Valentin Nouma Simba SC

Valentin Nouma Simba SC

Klabu ya Simba inatajwa kuwa kwenye mazungumzo na beki wa kushoto wa FC Saint Eloi Lupopo ya DR Congo, Valentin Nouma raia wa Burkina Faso mwenye umri wa miaka 24 kwaajili ya kuipata huduma yake Kuelekea Msimu Mpya wa 2024/2025.

Joyce Lomalisa Simba SC

Joyce Lomalisa Simba SC

Jean Othos Baleke Azam FC & Young Africans

Jean Othos Baleke Azam FC & Young Africans

Aliyekuwa Mshambuliaji wa Simba, Mkongomani, Jean Othos Baleke yupo nchini akiwa katika mazungumzo na timu mbili ambazo ni Azam FC na Young Africans

Inaelezwa kuwa Baleke aliyecheza Simba kwa mkopo akitokea TP Mazembe ya kwao DR Congo kabla ya kutimkia Al Ittihad ya Libya mwaka huu, yupo nchini kwaajili ya kukamilisha usajili wa kujiunga na kati ya Azam FC au Young Africans.

Edgar Wiliams Kengold FC

Edgar Wiliams Kengold FC

Klabu ya Pamba Jiji ya Jijini Mwanza iliyopanda Ligi Kuu Bara msimu huu wa 2024/2025 inaendelea kuboresha kikosi chake na sasa imetua kwa Mshambuliaji wa Ken Gold, Edgar Wiliams aliyeibuka kinara wa ufungaji kwenye Championship.

Victorien Adebayo & Mohamed Kamara Singida Black Stars FC

Victorien Adebayo & Mohamed Kamara Singida Black Stars FC

Klabu ya Singida Black Stars inadaiwa kuwa kwenye mazungumzo na Mshambuliaji Victorien Adebayo kutoka AS GNN ya kwako Nigeria pamoja na golikipa, Mohamed Kamara kutoka AC Horoya ya Guinea.

Adebayor aliyewahi kucheza RS Berkane na AmaZulu kabla ya kurejea kwao Niger anaitajika haraka ili kuziba nafasi ya Emmanuel Bola Labota anayetakiwa Young Africans.

Ayoub Lyanga Azam FC

Ayoub Lyanga Azam FC

Klabu ya Azam FC imedaiwa kuwa kwenye hatua nzuri ya kumuongezea mkataba mpya winga wake, Ayoub Lyanga ili asalie kikosini hapo.

Aboutwalib Mshery Young Africans

Aboutwalib Mshery Young Africans

Golikipa wa Klabu ya Yanga, Aboutwalib Mshery amemaliza mkataba wake na Klabu hiyo, wakati akisubiria hatma yake klabu ya Azam imetajwa Kuanza Mazungumzo naye.

Edward Charles Manyama Al Hilal Sudan

Edward Charles Manyama Al Hilal Sudan

Baada ya kumaliza mkataba wa kuitumikia Azam FC, beki Edward Charles Manyama ametajwa kuwaniwa Al Hilal ya Sudan na muda wowote anatatajiwa Kusaini Mkataba Mpya.

Klabu ya Dodoma Jiji imetajwa kuwa Katika hatua za mwisho kumsajili, Meck Mexime kwaajili ya kuchukuwa nafasi ya Francis Baraza aliyeachana na timu hiyo baada ya mkataba wake kumalizika

Mexime atajiunga na Dodoma Jiji baada ya kuachana na Singida Black Stars zamani Ihefu Fc.

Involata Mukoshi Fountain Gate Princess

Involata Mukoshi Fountain Gate Princess

Klabu za Simba Queens, Yanga Princess pamoja na Police Bullets ya Kenya zimepiga hodi kunako Fountain Gate Princess kuiwania saini ya kiungo Mkenya Involata Mukoshi ambaye anamaliza mkataba Msimu huu.

Athuman Masumbuko Mashujaa FC

Athuman Masumbuko Mashujaa FC

Mshambuliaji wa Mashujaa FC, Athuman Masumbuko amepanga kuachana na timu hiyo baada ya kutokuwa na msimu mzuri msimu ulioisha wa 2023/2024.

Najim Mussa Tabora United

Najim Mussa Tabora United

Uongozi wa Singida Black Stars umeingilia kati dili la kiungo wa Tabora United, Najim Mussa ambaye ametajwa kuwaniwa na timu mbalimbali zikiwemo za Simba SC na Azam FC.

Winifrida Gerald JKT Queens

Winifrida Gerald JKT Queens

Klabu ya Simba Queens imeanza mazungumzo ya kumnunua moja kwa moja winga wa JKT Queens, Winifrida Gerald anayemaliza mkataba mwishoni mwa mwezi huu.

Ian Otieno Zesco United

Ian Otieno Zesco United

Klabu ya Azam FC imeanza Mazungumzo na Klabu ya Zesco ya Zambia ili kuona uwezekano wa kumpata kipa, Ian Otieno kwaajili ya kuchukua nafasi ya Mohamed Mustafa aliyesajiliwa kwa mkopo kutoka Al-Merrikh ya kwao Sudan ambaye hawana uhakika wa kusajilia klabuni hapo.

Hussein Masalanga Ihefu FC

Hussein Masalanga Ihefu FC

Golikipa Hussein Masalanga rasmi ameachana na Ihefu Fc baada ya mkataba wake kutamatika ndani ya klabu hiyo.

Saido Ntibanzokinza Simba SC

Saido Ntibanzokinza Simba SC

Kiungo wa klabu ya Simba SC, Saido Ntibanzokinza raia wa Burundi ameachana rasmi na Klabu hiyo.

Malickou Ndoye, Issah ndala, Ali Ahmada

Malickou Ndoye, Issah ndala, Ali Ahmada

Klabu ya Azam Fc imeachana na beki wake Malickou Ndoye, Azam pia inatarajiwa kuachana na Abdulai Idrisu, Issah ndala pamoja na Ali Ahmada.

Jonas Mkude, Kibwana Shomari, Bakari Nondo Mwamnyeto, Salum Abubakar

Jonas Mkude, Kibwana Shomari, Bakari Nondo Mwamnyeto, Salum Abubakar

Klabu ya Yanga sc imepanga kuwaongeza mikataba mipya wachezaji Salum Abubakar, Jonas Mkude, Bakari Nondo Mwamnyeto pamoja na Kibwana Shomari.

Cheikh Sidibe Azam FC

Cheikh Sidibe Azam FC

Mchezaji Cheikh Sidibe ameomba kuondoka ndani ya Klabu ya Azam Fc.

Mohamed Mustapha Azam FC

Mohamed Mustapha Azam FC

Golikipa wa klabu ya Azam FC, Mohamed Mustapha atarejea kwenye klabu yake ya Al Mereikh dirisha lijalo la Usajili baada ya mkopo wa miezi 6 kuisha.

Goran Kopunovic Pamba Jiji FC

Goran Kopunovic Pamba Jiji FC

Klabu ya Pamba Jiji iliyopanda Ligi Kuu ipo mbioni kumsajili aliyewahi kuwa Kocha wa Vilabu vya Simba SC na Tabora United, Goran Kopunovic.

Yusuph Kagoma Simba SC

Yusuph Kagoma Simba SC

Kiungo, Yusuph Kagoma yupo mbioni kujiunga na klabu Simba SC akiwa Mchezaji huru baada ya kuachana na Singida Fountain Gate FC.

Salum Athuman ‘Stopper’ Simba SC

Salum Athuman ‘Stopper’ Simba SC

Klabu ya Simba inajaribu kufanya mazungumzo ya kumsajili beki wa KVZ ya Zanzibar, Salum Athuman ‘Stopper’ ambaye amekuwa na kiwango bora.

Brian Mandela Onyango Simba SC

Brian Mandela Onyango Simba SC

Klabu ya Simba inamuwania beki wa kati wa Mamelodi Sundown ya Afrika Kusini raia wa Kenya, Brian Mandela Onyango mwenye miaka 29.

Seif Abdallah Karihe Mashujaa FC

Seif Abdallah Karihe Mashujaa FC

Klabu ya Mashujaa FC imetajwa Kuanza Mazungumzo na aliyekuwa mshambuliaji wa Mtibwa Sugar, Seif Abdallah Karihe ili kuziba nafasi ya Adam Adam aliyerejea Azam FC.

Yannick Bangala Azam FC

Yannick Bangala Azam FC

Viongozi wa Simba wametajwa kufanya mawasiliano na wakala wa kiungo, Yannick Bangala anayeichezea Azam FC ili kuangalia uwezekano wa kumpata nyota huyo wa zamani ya Young Africans.

Farid Mussa Yanga SC

Farid Mussa Yanga SC

Klabu ya Azam FC imetajwa kuanza mazungumzo ya kumrejesha winga wa zamani wa timu hiyo, Farid Mussa aliyemaliza mkataba huko Young Africans.

Yona Amosi Tanzania Prisons FC

Yona Amosi Tanzania Prisons FC

Golikipa Yona Amosi yupo huru baada ya mkataba wake kumalizika ndani ya timu yake ya Tanzania Prisons FC.

Pa Omar Jobe Simba SC

Pa Omar Jobe Simba SC

Klabu ya Simba huenda ikaachana mshambuliaji wake, Pa Omar Jobe mazungumzo yanakaribia kukamilika.

Erick Johora Mashujaa FC

Erick Johora Mashujaa FC

Klabu ya Mashujaa ipo kwenye mazungumzo ya kumuongeza mkataba mpya golikipa wake, Erick Johora.

Kipa huyo wa zamani wa vilabu vya Eagle Noir na Yanga sc alijiunga na Mashujaa Kwa mkataba wa miezi 6 akitokea Geita Gold

Sebu Sebu Geita Gold

Sebu Sebu Geita Gold

Klabu ya Dodoma Jiji imetajwa kutuma ofa ya kuhitaji golikipa, Sebu Sebu baada mkataba wake kumalizika ndani ya klabu ya Geita Gold.

Geofrey Muha Geita Gold

Geofrey Muha Geita Gold

Vilabu vya KMC FC, Kengold, na Tanzania Prisons vinaiwania Saini ya beki Geofrey Muha baada ya mkataba wake na Geita Gold kumalizika.

Derrick Mukombozi Namungo FC

Derrick Mukombozi Namungo FC

Uongozi wa Simba SC upo kwenye mazungumza ya kunasa saini na beki wa Namungo na timu ya taifa ya Burundi, Derrick Mukombozi kwaajili ya kuziba pengo la Henock Inonga ambaye anatajwa kutaka kuondoka klabuni hapo.

Amina Bilal Yanga Princess

Amina Bilal Yanga Princess

Klabu ya Yanga Princess imeanza maandalizi mapema ya msimu ujao baada ya kumfuata kiungo wa JKT Queens, Amina Bilal ambaye mkataba wake unaisha mwishoni mwa msimu huu.

Deusdedith Okoyo Pamba Jiji FC

Deusdedith Okoyo Pamba Jiji FC

Kuna uwezekano mkubwa wa beki wa kushoto, Deusdedith Okoyo akajiunga na Pamba Jiji ya Jijini Mwanza iliyopanda daraja msimu huu.

Richaldson Ng'odya Kagera Sugar FC

Richaldson Ng’odya Kagera Sugar FC

Klabu ya JKT Tanzania imeanza hesabu za usajili wa winga wa Kagera Sugar FC, Richaldson Ng’odya.

Kenneth Semakula Simba SC

Kenneth Semakula Simba SC

Klabu ya Simba ipo kwenye mazungumzo na aliyekuwa kiungo wa SC Villa ya Uganda, Kenneth Semakula ili kujiunga nao msimu ujao.

Kennedy Juma Simba SC

Kennedy Juma Simba SC

Klabu ya Coastal Union imeanza hesabu za kumnasa beki wa Simba, Kennedy Juma baada ya mkataba wake kumalizika msimu huu.

Hiyo inatokana na kuondokewa na beki wa kikosi hicho, Lameck Lawi ambaye tayari msimu ujao atajiunga na Simba baada ya kufikia makubalino baina ya timu hizo na kusainishwa mkataba wa miaka miwili.

Austin Odhiambo Singida Black Stars

Austin Odhiambo Singida Black Stars

Klabu ya Singida Black Stars, inawania saini ya kiungo mshambuliaji wa Gor Mahia, Austin Odhiambo kwaajili ya kujiunga nao msimu ujao.

Taarifa zinaeleza nyota wawili wa Kenya, Elvis Rupia na Duke Abuya ndio ambao wanatumika kama chambo cha kumshawishi kiungo huyo japo changamoto kubwa inayoweza kutokea ni kutokana na Gor Mahia kufuzu Ligi ya Mabingwa.

Saidi Zanda Stand United FC

Saidi Zanda Stand United FC

Kiungo Mshambuliaji, Saidi Zanda yupo huru baada ya mkataba wake na klabu ya Stand United ya mkoani shinyanga inayoshiriki Championship kumalizika.

Hashimu Manyanya Namungo FC

Hashimu Manyanya Namungo FC

Baada ya kuitumikia Namungo Kwa takribani misimu mitano (5) mfululizo Hashimu Manyanya yupo huru baada ya mkataba wake kutamatika mwishoni mwa msimu uliopita.

Taarifa ambazo Nijuze Habari inazo hadi Sasa hakuna mazungumzo yaliyofanyika kuhusu kuongezewa mkataba mpya na klabu hiyo.

Yusuph Valentino Mhilu Kagera Sugar FC

Yusuph Valentino Mhilu Kagera Sugar FC

Yusuph Valentino Mhilu yupo huru baada ya mkataba wake na Geita Gold kutamatika tangu May 2024.

Muhilu amekulia Kwenye timu ya vijana ya Yanga Sc, pia amewahi itumukia Kagera Sugar Kwa nyakati tofauti

Eliud Ambokile Mbeya City

Eliud Ambokile Mbeya City

Mashambuliaji wa Zamani wa TP Mazembe ya DR Congo, Eliud Ambokile ni mchezaji huru baada ya mkataba wake kumalizika ndani ya klabu ya Mbeya City inayoshiriki Championship.

Mohamedi Hussein Mudi Colour dodoma jiji

Mohamedi Hussein Mudi Colour dodoma jiji

Golikipa, Mohamedi Hussein maarufu kwa jina la Mudi Colour yupo huru baada kumaliza mkataba wake na Dodoma Jiji FC ya Dodoma.

Salum Kihimbwa Mtibwa Sugar

Salum Kihimbwa Mtibwa Sugar

Mshambuliaji wa zamani wa vilabu vya Mtibwa Sugar, Dodoma Jiji na Tanzania Prisons, Salum Kihimbwa ni mchezaji huru.

Erick Kyaruzi Mopa Geita Gold

Erick Kyaruzi Mopa Geita Gold

Beki wa Geita Gold, Erick Kyaruzi maarufu Mopa amemaliza mkataba wake ndani ya timu hiyo hivyo yupo huru.

Haruna Kassim Shabani Tiote Mtibwa Sugar

Haruna Kassim Shabani Tiote Mtibwa Sugar

Mkataba wa Haruna Kassim Shabani maarufu Tiote na Mtibwa Sugar umemalizika na Sasa ni mchezaji huru.



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz