Gamondi hataki utani awapa masharti haya wachezaji wake wakienda likizo - EDUSPORTSTZ

Latest

Gamondi hataki utani awapa masharti haya wachezaji wake wakienda likizo

 

Leo ndio leo ni ZAMBIA vs TANZANIA usikose kuitazama mechi hii live kabisa bure kwenye simu yako bonyeza hapa kudownload app itakayorusha mechi hii live buree pia ndani ya app hii kuna muvi zilizo tafsiriwa kwa kiswahili na chanel za azam tv na Dstv bofya sasa kuidownload bure

Licha ya kupewa mapumziko ya mwezi mmoja, wachezaji wa Yanga wamepewa program maalum ya mazoezi ambayo watapaswa kufanya wakiwa makwao

Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi amefichua kuwa hataki kuanza tena upya pale likizo itakapomalizika

Gamondi ambaye hivi karibuni alisaini mkataba wa kuendelea kuwatumikia mabingwa hao wa Tanzania Bara, amesema wanahitaji kuwa bora zaidi msimu ujao ili kuhakikisha wanalinda kile walichonacho na kupata mafanikio zaidi

"Kila mchezaji anatakiwa kupumzika lakini hatuwezi kwenda kupumzika moja kwa moja kila mchezaji aliyemaliza msimu hapa amepewa ratiba ambayo anatakiwa kuitekeleza na kila wakati atawasilisha kwa kocha wa mazoezi"

"Hili ni muhimu sana kwa kila mchezaji kuzingatia kinyume na hapo tutakuwa wakali kwa lengo la kutokuwa na kazi ngumu kwenye maandalizi ya mwanzo wa msimu, nimeambiwa muda hautakuwa wa kutosha sana lazima tujipange," alisema Gamondi 

Baada ya ratiba ya michuano ya Kagame Cup kutolewa ambapo Yanga imethibitisha kushiriki michuano hiyo inayoanza Julai 06, huenda Yanga ikarejea kambini mapema kwa ajili ya maandalizi ya michuano hiyo itakayoshirikisha timu 16

BONYEZA HAPA KUTAZAMA VIDEO ZA WAKUBWA UJIFUNZE MAUTUNDU YA CHUMBANI



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz