Alicho kisema Ahmed Ally baada ya simba kukubali kichapo kutoka kwa Dodoma Jiji - EDUSPORTSTZ

Latest

Alicho kisema Ahmed Ally baada ya simba kukubali kichapo kutoka kwa Dodoma Jiji

Tunapaswa Simba kujitathimini - Ahmed Ally

Ni leo Dodoma Jiji vs Yanga usikose kuitazama mechi hii Live bureee kupitia simu yako bonyeza hapa kudownload app inayirusha mechi hii bure kabisa

Meneja wa Habari na Mawasiliano wa Simba SC, Ahmed Ally, asema kutokana na matokeo wanayoyapata, wanapaswa kujitathimini kabla ya msimu kuisha.

Akizungumza jana mara baada ya kufurushwa kwenye mashindano ya CRDB Confederation Cup na Mashujaa FC, Ahmed alisema, anawapa Pole mashabiki wote wa Simba na kikubwa kwa sasa ni kila mmoja kujitathimini.

"Sisi viongozi tunapaswa kujitathimini, benchi la ufundi, wachezaji kila mmoja anapaswa kujitathimini kuona je tunakosea wapi na nini tufanye kurekebisha kabla ya kufanya tathimini ya jumla mwisho wa msimu," alisema Ahmed.

Ahmed alisema, kama taasisi ilikuwa na malengo ya kuchukua vikombe ambavyo vingi tayari wamevipoteza na wamebakiwa na Ligi Kuu pekee hivyo wanapaswa kufanya mabadiliko makubwa mwishoni mwa msimu.



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz