AZAM FC WAMJIBU DUBE- ISSUE IKO HIVI.. - EDUSPORTSTZ

Latest

AZAM FC WAMJIBU DUBE- ISSUE IKO HIVI..

AZAM FC  WAMJIBU DUBE- ISSUE IKO HIVI..

Uongozi wa Azam FC umesemna kuwa hakuna tena nafasi kwa Mshambuliaji wa timu hiyo, Prince Dube kurejea katika kikosi na kuanzia sasa umefunga mjadala wake hadi atakapokamilisha uvunjaji wa mkataba.

JIUNGE NA GROUP LA WAKUBA HAPA 18+ HAPA


PATA GB 30 KILA MTANDAO BURE  HAPA

Kauli hiyo ya Azam FC imekuja muda mfupi baada ya kuripotiwa kuwa Dube ana mpango wa kurejea kikosini ili kuungana na wenzake baada ya mwanzoni mwa juma hili kukutana na kocha Yousouf Dabo na kufanya naye mazungumzo.

Habari za uhakika kutoka ndani ya uongozi wa Azam FC zimelithibitisha kuwa vigogo wa timu hiyo wamepiga marufuku kwa Dube kuhudhuria mazoezi au kushiriki shughuli zozote za timu hiyo na wanachohitaji ni mchezaji huyo kulipa kiwango wanachohitaji kwa ajili ya kuvunja mkataba wake.

“Hili jambo limewaudhi sana viongozi wa juu wa Azam FC ambao wametoa agizo kuwa Dube asiruhusiwe kuwepo kwenye timu hadi pale atakapokamilisha suala la kuvunja mkataba wake, iwe kwa yeye mwenyewe kuleta fedha ambazo zinatakiwa au klabu inayomtaka ije mezani.

“Wanafahamu ujanja ambao umeanza kutumika hivyo hawataki kuruhusu utokee kwani utaivuruga timu na isitoshe hata wachezaji wenzake hawajafurahishwa na hicho anachokifanya kimesema chanzo kutoka Azam FC.

Hilo limethibitishwa na Afisa Habari wa Azam FC, Thabit Zakaria ‘Zaka Zakazi’ kwa kusema kuwa wamefunga rasmi ukurasa wa mshambuliaji huyo.

“Azam FC imeshafunga mjadala wa Prince Dube. Kuanzia hatutolijadili tena suala lake hadi pale kile ambacho Azam FC inachokihitaji kitatimizwa.

“Dube bado hajarejea na hatorejea kikosini na ukurasa wake na Azam FC umeshafungwa rasmi,” amesema Zaka.

JIUNGE NA GROUP LA WAKUBA HAPA 18+ HAPA


PATA GB 30 KILA MTANDAO BURE  HAPA

Juzi Dube alizungumza kwa kifupi kuwa mengi atayasema baada ya sakata lake na klabu hiyo kumalizika.

Kuna mambo mengi hamuyajui, wakati ukifika mtayajua kwa sasa niacheni kwanza nitafakari,” amesema Dube.



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz