Jesus Moloko amaliza kifungo chake - EDUSPORTSTZ

Latest

Jesus Moloko amaliza kifungo chake

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Winga wa Yanga Jesus Moloko amemaliza adhabu ya kufungiwa mechi tatu na sasa yuko tayari kwa mchezo wa fainali ya Ngao ya Jamii dhidi ya Simba ambao utapigwa Jumapili, August 13 katika uwanja wa Mkwakwani


Adhabu hiyo aliipata msimu uliopita baada ya kuonyeshwa kadi nyekundu kwenye mchezo wa ligi kuu dhidi ya Mbeya City uliopigwa uwanja wa Sokoine na kumalizika kwa matokeo ya sare ya mabao 3-3


Moloko alikosa michezo dhidi ya Tanzania Prisons (Ligi Kuu) na mechi mbili dhidi ya Azam Fc kuanzia mchezo wa fainali ya kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) msimu uliopita na nusu fainali ya Ngao ya Jamii


Hii ni habari njema kwa Kocha Mkuu wa Yanga Miguel Gamondi ambaye atakuwa na machaguo mengi katika eneo la winga kuelekea mchezo dhidi ya Simba siku ya Jumapili mechi itakuwa mubashara kwenye app YETU kama bado hujaipakua BOFYA HAPA



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz