Walicho kisema Yanga baada ya kupangwa na Asas Fc ligi ya Mabingwa Africa - EDUSPORTSTZ

Latest

Walicho kisema Yanga baada ya kupangwa na Asas Fc ligi ya Mabingwa Africa

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Afisa Habari wa Yanga Ali Kamwe amesema malengo ya chini katika michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika inayotarajiwa kuanza mwezi ujao ni kutinga hatua ya makundi


Katika droo ya mechi za awali na raundi ya kwanza ambayo ilifanyika jana huko Misri, Yanga imepangwa kuanzia Djibout kuikabili Asas Fc


Mechi ya mkondo wa kwanza itapigwa kati ya August 15-20 na mechi ya marudiano itapigwa wiki moja baadae jijini Dar es salaam


Kama Yanga itafanikiwa kufuzu hatua ya awali kwenye raundi ya kwanza itacheza dhidi ya mshindi wa mechi kati ya Otoho Fc ya Congo dhidi ya Al Marreikh ya Sudan


Katika raundi ya kwanza pia Yanga itaanzia ugenini na kumalizia mechi ya pili nyumbani


Kamwe amesema wanajiandaa kwa mechi hizo na jambo muhimu ni kuwaheshimu wapinzani wao


"Sisi kama Yanga Africans tumeipokea vizuri droo iliyopangwa na Shirikisho la Mpira wa Miguu barani Afrika. Nataka niwaambie Wanachama na mashabiki wetu kuwa hakuna timu ndogo kwenye Ligi ya Mabingwa, kila timu inajiandaa ili kuweza kufanya vizuri"


"Tuna muda mrefu sana hatujacheza hatua ya makundi ya Ligi ya Mabingwa barani Afrika. Msimu uliopita ulikuwa mzuri kwetu tukifanikiwa kucheza fainali ya kombe la Shirikisho la CAF. Msimu huu malengo ya klabu ni kuona kwanza tunatinga hatua ya makundi"


"Nawaomba Wanachama na Mashabiki wetu tuhamishe nguvu zetu kwenye michuano hii, tuhakikishe tunacheza hatua ya makundi," alisema Kamwe



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz