Singida yajibu kupewa jina la Yanga B, Simba B - EDUSPORTSTZ

Latest

Singida yajibu kupewa jina la Yanga B, Simba B

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Kufuatia Klabu ya Singida Fountain Gate kumsajili aliyekuwa beki wa Klabu ya SImba, Joasha Onyango kwa mkopo, Msemaji wa klabu hiyo, @massanzajr amesema;


YANGA B


Tuliposajili wachezaji wengi kutoka Yanga msimu uliopita, ukijumlisha na kupoteza mechi dhidi ya Yanga, tuliitwa Yanga B. Ni maneno ya kukera lakini ndio mashabiki walivyo. Tunavumilia.


SIMBA B


Tunaanza msimu mpya na tayari maneno yameanza kusambaa kwamba Singida ni Simba B. Kisa tu zipo taarifa za chini kwa chini kuwa 'tunapewa' wachezaji na Simba SC.


UKWELI UKOJE?


Ni dhahiri bado watanzania wapo kwenye ulevi wa Simba na Yanga. Sisi kama timu ya kizazi kipya tunaona tunao wajibu wa kubadilisha fikra hizi za kizamani. Ni ngumu lakini tutafanikiwa.


Singida FG tunathubutu kusajili wachezaji bora kutoka vilabu vyote ndani na nje ya nchi kulingana na mahitaji yetu. Timu yetu ni chotara. Tutasajili bila kujali wanazi wa soka watasemaje, malengo yetu kwanza.


Tumedhamiria kuleta ushindani ligi kuu na hata kimataifa. Ni dhamira inayopaswa kuungwa mkono na kila mpenda maendeleo ya soka. Ushabiki wa kizamani hauna nafasi tena. Tutazame picha kubwa.


Maendeleo hayana chama!



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz