Ally kamwe awatuliza Mashariki wa Yanga "wakati wa furaha umewadia" - EDUSPORTSTZ

Latest

Ally kamwe awatuliza Mashariki wa Yanga "wakati wa furaha umewadia"

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Afisa Habari wa Yanga Ali Kamwe amesema wako tayari kuanza utambulisho wa wachezaji wapya hivyo Wananchi wakae tayari


Kamwe amesema taratibu zote za ndani zimeshakamilika


"Leo ni siku ya mapumziko lakini si unaona tuko kazini?Tunaweka mambo sawa ili tuanze kutambulisha wachezaji wetu"


"Tumewasikia Wanachama wetu wanalalamika, wamechoka kusubiri, Rais ametuagiza tutambulishe wachezaji, tuko tayari"


"Tuliwaahidi baada ya kocha kuwasili tutawatangazia benchi la ufundi, zoezi ambalo tutalifanya wakati wowote"


"Kama tulivyosema tangu mapema, usajili wetu tulishaukamilisha muda mrefu, sasa wakati wa kuwafahamu wachezaji umefika," alisema Kamwe


Kulingana na taarifa ambayo iliyotolewa na Yanga mapema wiki hii, wachezaji wanapaswa kuripoti kambini Avic Town siku ya kesho Jumatatu, Julai 10


Ni takribani wiki nne zimebaki kabla ya msimu wa 2023/24 kuanza ambapo mechi za Ngao ya Jamii zitaanza August 09 Yanga ikichuana na Azam Fc



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz