Mayele atetema Gabon - EDUSPORTSTZ

Latest

Mayele atetema Gabon

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Mshambuliaji wa Yanga Fiston Mayele jana aliisaidia DR Congo kupata ushindi wa mabao 2-0 ugenini dhidi ya Gabon katika mchezo wa kuwania kufuzu fainali za Afcon 2023


Mayele aliyeingia kwenye dakika ya 74, alifunga bao la pili la DR Congo kwenye dakika ya 83 baada ya kuwachambua walinzi wa Gabon kabla ya kuujaza mpira kimiani


Baada ya kuuweka mpira kimiani Mayele alishangilia kwa staili yake ya kutetema huku wachezaji wote wa DR Congo wakiungana nae kutetema


Jana nyota nane wa Yanga walikuwa uwanjani kuzitumikia timu zao za Taifa


Bakari Nondo Mwamnyeto, Dickson Job, Ibrahim Bacca na Mudathir Yahya waliitumikia Taifa Stars katika mchezo dhidi ya Niger uliopigwa uwanja wa Benjamin Mkapa na Tanzania kushinda bao 1-0


Khalid Aucho akaitumikia Uganda katika mchezo dhidi ya Algeria wakati Djigui Diarra akiwa langoni katika mchezo dhidi ya Congo (Brazaville)


Stephane Aziz Ki akaanza katika mchezo dhidi ya Cape Verde



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz