Hersi Said: Tutamsajili yoyote Afrika - EDUSPORTSTZ

Latest

Hersi Said: Tutamsajili yoyote Afrika

 

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA.

Rais wa Mabingwa wa Soka Tanzania Bara Injinia Hersi Said, amepiga mkwara mzito kuhusu masuala ya usajili akiweka wazi kuwa jina lolote atakalopewa atafanyia kazi kuhakikisha anamleta mchezaji huyo.


Injinia Hersi alifanikisha madili ya wachezaji wengi ndani ya kikosi cha Young Africans akiwemo Stephane Aziz KI ambaye alikuwa anakipiga ASEC Mimosas ya Ivory Coast.


Aziz Ki alikuwa anatajwa kuwa kwenye rada za mabosi wa Simba pamoja na Azam FC, jambo lililoongeza presha kwenye kuisaka saini yake na mwisho aliibuka Young Africans.


Injinia Hersi amesema: “Kwenye suala la usajili, Young Africans tupo tofauti na tunazidi kuiboresha sekta hii kutokana na kuwa na mfumo wa mabadiliko, hivyo wakishafanya mchakato wao ninawaambia tu jina lolote wanipe.


“Wakinipa jina la mchezaji ambaye wanamuhitaji popote kule hizo ndizo kazi zangu, nitahakikisha ninakamilisha hilo dili na kuwapatia mchezaji wao.”


Chanzo: Dar24



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz