Breaking: Aishi Manula nje miezi minne, kurejea nchini kesho - EDUSPORTSTZ

Latest

Breaking: Aishi Manula nje miezi minne, kurejea nchini kesho

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Golikipa namba moja wa Simba SC, Aishi Manula, atakuwa nje kwa miezi minne baada ya kufanyiwa upasuaji wa nyama za paja.


Aishi alipata majeraha katika mechi ya robo fainali ya kombe la Azam Sports Federation dhidi ya Ihefu FC iliyochezwa Aprili 7, mwaka huu katika Uwanja wa Benjamini Mkapa jijini Dar.


Upasuaji huo alifanyiwa Mei 30, 2023 nchini Afrika Kusini ambapo kwa mujibu wa Simba APP, golikipa huyo namba moja wa Taifa Stars, atarejea kesho na kuendelea na sehemu ya pili ya mazoezi ya viungo ili aweze kupona vizuri.


"Atakuwa nje kwa takriban miezi minne akifanya mazoezi ya viungo ili jeraha lipone vizuri," alisema daktari wa timu Edwin Kagabo.



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz