Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA
Chivaviro anatarajiwa kuachana na Marumo mwishoni mwa msimu baada ya timu hiyo kushuka daraja kipaumbele chake kikiwa kujiunga na timu ambayo itashiriki michuano ya CAF msimu ujao
Katika moja ya mahojiano na vyombo vya Habari Afrika Kusini, Rais wa Yanga Injinia Hersi Said aliahidi kuwa Yanga itasajili mshambuliaji mmoja kutoka ligi kuu ya Afrika Kusini
Khanyisa Mayo wa Cape Town City na Ranga Chivaviro ndio wachezaji waliokuwa wakilengwa na Injinia Hersi
Jana Wakala wa Chivaviro akathibitisha kuwepo kwa mazungumzo kati yao na Yanga huku akieleza kuwa Chivaviro amevutiwa zaidi na ofa iliyotolewa na Yanga licha ya Azam Fc nayo kumuhitaji
Chivaviro ni mmoja wa washambuliaji waliofanya vizuri katika ligi kuu ya Afrika Kusini msimu huu licha ya timu yake ya Marumo Gallants kushuka daraja
Amefunga jumla ya mabao 16, akifunga mabao 10 kwenye ligi na mabao sita kwenye kombe la Shirikisho sawa na Fiston Mayele wa Yanga
Mayo na Peter Shalulile ndio vinara wa mabao ligi kuu ya Afrika Kusini kila mmoja akifunga mabao 12
Ikiwa imetinga fainali ya kombe la Shirikisho msimu huu, Yanga inajipanga kuhakikisha msimu ujao inafanya vyema katika michuano ya Ligi ya Mabingwa
No comments:
Post a Comment