PSG wachezea kichapo nyumbani, Hakimi alambwa kadi nyekundu - EDUSPORTSTZ

Latest

PSG wachezea kichapo nyumbani, Hakimi alambwa kadi nyekundu

Ofa ya Bando la Internet wiki BURE Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Klabu ya PSG wamepokea kichapo cha mabao 3-1 dhidi ya Lorient hapo jana ambapo baada ya Achraf Hakimi kutolewa nje kwa kadi nyekundu walibaki 10 pekee uwanjani na kuwafanya timu pinzani kupata wigo mpana wa kuwashambulia.


Kutolewa kwa Achraf Hakimi dakika ya 20 kwa kadi ya pili ya njano kulitoa nafasi kwa Enzo Le Fee kuwapatia wageni bao la kwanza la kustukiza katika dimba la Parc de Princess.


Ingawa Kylian Mbappe aliwarudisha PSG mchezoni baada ya kusawazisha kwa bao la utata lakini Lorient walishambulia kwa kasi na kupata mabao mengine mawili yakiwekwa wavuni na Darlin Yongwa na Bamba Dieng.



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz