Manula kutibiwa Africa kusini - EDUSPORTSTZ

Latest

Manula kutibiwa Africa kusini

Pata 50,000 BURE Kila Siku Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Mlinda lango namba moja wa Simba na timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifa Stars' Aishi Manula anatarajiwa kupelekwa Afrika Kusini kwa ajili ya matibabu zaidi baada ya kuumia akiwa kwenye majukumu na klabu yake


Manula aliumia kwenye mchezo wa robo fainali kombe la FA dhidi ya Ihefu Fc, mchezo ambao Simba ilishinda mabao 5-0


Meneja wa Manula Jemedari Said amesema bado mchezaji huyo anauguza jeraha na klabu ya Simba inajiandaa kumpeleka Afrika Kusini kwa ajili ya matibabu zaidi 


"Mchezaji ni wa klabu kwa hiyo mwenye jukumu la kumtibu ni klabu yake ya Simba. Tayari taratibu zimeshafanyika na muda si mrefu atapelekwa kwenye matibabu wiki hii"


"Amepelekwa Muhimbili, ikaonekana kuna damu imevuja kwa ndani na madaktari wakabaini msuli umekatika kwa hiyo anahitaji upasuaji ambapo utafanyika nje ya nchi," alisema Jemedari



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz