Akaminko kuondoka Azam fc??? - EDUSPORTSTZ

Latest

Akaminko kuondoka Azam fc???

Ofa ya Bando la Internet wiki BURE Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Ofisa Mtendaji Mkuu (CEO) wa Azam FC Abdulkarim Amin ‘Popat, amesema kiungo wa timu hiyo, Mghana James Akaminko bado yupo sana Azam na haondoki.


Popat amesema licha ya mchezaji huyo kuhitajika na baadhi ya timu, bado yupo kwenye mipango ya muda mrefu, ivyo hawapo tayari kumuweka sokoni kwa sasa.


“Ndio kwanza tumemsajili msimu huu, na sisi tuna shida naye, hatuwezi kumuachia kirahisi, halafu mwisho wa siku watu waendelee kuuliza Azam FC inakwama wapi?


“Hatuwezi kusema tunaijenga timu halafu tumuachie mchezaji bora, hiyo inakurudisha nyuma na kuanza moja, hata kama ni biashara ni lazima uangalie na mahitaji yako.”


Nyota huyo ambaye amejizolea umaarufu mkubwa katikati ya dimba amekuwa akihusishwa na kutakiwa na timu mbalimbali nchini, huku baadhi zikitajwa kupeleka ofa rasmi ya kumtaka.



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz