Var kufungwa Kwa mkapa Mechi ya Simba vs Wydad - EDUSPORTSTZ

Latest

Var kufungwa Kwa mkapa Mechi ya Simba vs Wydad

Ofa ya Bando la Internet wiki BURE Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Shirikisho la soka barani Afrika (CAF) limethibitisha kutumika kwa teknolojia ya usaidizi wa waamuzi kwa njia ya video (VAR) katika mechi za robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa na kombe la Shirikisho barani Afrika


Klabu za Tanzania Simba na Yanga zitakuwa kwenye majukumu ya kupeperusha bendera ya nchi mwishoni mwa wiki hii kwenye mechi hizo za robo fainali


Jumamosi April 22 katika uwanja wa Benjamin Mkapa, saa 10 jioni Simba itawakabili mabingwa watetezi wa ligi ya mabingwa Wydad Athletic, VAR itatumika katika mchezo huu wa mkondo wa kwanza na pia itatumika katika mchezo wa mkondo wa pili utakaopigwa Morocco April 29


Jumapili April 23, Yanga itakuwa ugenini huko Nigeria kuikabili Rivers United katika mchezo wa mkondo wa kwanza kombe la Shirikisho, VAR pia itatumika


Mchezo wa marudiano utapigwa uwanja wa Benjamin Mkapa, April 30 ambapo teknolojia ya VAR pia itatumika



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz