Dk Tulia Ackson naye ajitosa kujinusuru Mbeya City - EDUSPORTSTZ

Latest

Dk Tulia Ackson naye ajitosa kujinusuru Mbeya City

Ofa ya Bando la Internet wiki BURE Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Spika wa Bunge la Tanzania Dk Tulia Ackson ametoa Sh2 milioni kwa timu ya Mbeya City ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya timu hiyo kuelekea mchezo dhidi ya Kagera Sugar Aprili 23


Fedha hizo zimetolewa leo Aprili 18, 2023 wakati wa Chakula cha mchana kilichoandaliwa na Spika kwa wachezaji wa Mbeya City jijini Dodoma wakiwa safarini kuelekea Bukoba kwa ajili ya mechi itayochezwa uwanja wa Kaitaba


Akikabidhi zawadi hiyo kwa niaba ya Dk Tulia, mbunge Lupa Chunya Masache Kasaka kwa kushirikiana na wabunge wa Mbeya nao wametoa Sh1 milioni na kufanya jumla kuwa Sh3 milioni.


Wabunge hao pia wameahidi kununua ushindi kwa timu ya Mbeya City kwa kila mechi zilizosalia kwenye ligi Kuu ya Tanzania inayoendelea


Hivi karibuni Mbunge wa zamani wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi 'Sugu' aliahidi kutoa Tsh Milioni 1 kwa kila bao la ushindi litakalofungwa na Mbeya City katika mechi zilizobaki


Mbeya City inashika nafasi ya 13 kwenye msimamo wa ligi kuu ya NBC ikiwa na alama 27 ikiwa ni alama saba juu ya eneo la kushuka daraja


Hata hivyo kama watamaliza katika nafasi hiyo, watacheza play-off



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz