Tutawashangaza wydad - Kocha Roberthino - EDUSPORTSTZ

Latest

Tutawashangaza wydad - Kocha Roberthino

Ofa ya Bando la Internet wiki BURE Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira amesema wamejiandaa kuwashangaza Wydad Athletic katika mchezo wa mkondo wa pili robo fainali ya ligi ya mabingwa barani Afrika


Simba itakuwa ugenini siku ya Ijumaa, April 28 katika mchezo utakaopigwa uwanja wa Mohammed V, saa 3 usiku kwa saa za Tanzania


Akizungumza katika Mkutano na Wanahabari mapema leo, Robertinho alisema amekiandaa kikosi chake kimbinu kukabiliana na Wydad katika mchezo muhimu wa kuwania tiketi ya kutinga nusu fainali


"Tutawashangaza wapinzani wetu kwa sababu tumefanya kazi kubwa kufika hapa tulipo, tumekuwa tukibadili mazoezi kulingana na mpinzani tunayekutana nae"


"Binafsi ningependa tushinde magoli mawili au matatu lakini hata goli moja litatufaa kutokana na kile tulichokipata kwenye mchezo wa kwanza"


"Nina imani kubwa na wachezaji wangu na viongozi kwa ujumla, tumejiandaa kikamilifu kuelekea mchezo huu. Tumekuwa na mfululizo wa matokeo mazuri, hili ni jambo muhimu kwetu," alisema Robertinho


Nae kiungo mshambuliaji Pape Ousmane Sakho alisema hawana hofu yoyote kuelekea mchezo huo, wamefanya maandalizi kabamba kuhakikisha wanashinda


Sakho amesema hawana hofu na mashabiki wa Wydad zaidi vurugu zao zitawaongezea ari ya kupambana



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz