Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA
Droo ya robo fainali kombe la Shirikisho Barani Afrika imefanyika leo huko Misri ambapo kwa mara nyingine, Yanga imepangwa kuchuana na Rivers United ya Nigeria
Ni hawa hawa Rivers United ambao msimu uliopita waliiondosha Yanga kwenye hatua ya awali michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika
Hii ni nafasi kwa Yanga kulipa kisasi,mechi ya kwanza robo fainali itapigwa Nigeria na mechi ya pili kupigwa uwanja wa Benjamin Mkapa
Aidha kama Yanga itatinga nusu fainali, katika hatua hiyo itachuana na mshindi wa mchezo kati ya Pyramids dhidi ya Malumo Galants
RATIBA KAMILI
Pyramids Fc vs Malumo Galants - QF1
US Monastir vs ASEC Mimosas - QF2
USM Alger vs AS FAR Rabat - QF3
Rivers United vs Yanga - QF4
NUSU FAINALI
QF4 vs QF1 - SF1
QF2 vs QF3 - SF2
FAINALI
SF1 vs SF2
No comments:
Post a Comment