Tetesi za usajili barani ulaya Leo Alhamisi - EDUSPORTSTZ

Latest

Tetesi za usajili barani ulaya Leo Alhamisi

Kuingiza pesa Mtandaoni bure Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Leicester wanahitaji takriban pauni milioni 50 kumuuza kiungo mshambuliaji wa England James Maddison, huku Tottenham wakipewa nafasi kubwa ya kumsajili mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 26. (Telegraph – Subscription Required)


Inter Miami wako tayari kumpa mshambuliaji wa Paris St-Germain na Argentina Lionel Messi, 35, hisa za usawa katika klabu hiyo ili kumshawishi ajiunge msimu huu wa joto. (Independent)


Meneja wa klabu ya Bayer Leverkusen ya Uhispania Xabi Alonso ameibuka kuwania nafasi ya kuinoa Chelsea baada ya Graham Potter kutimuliwa. (Guardian)


Arsenal wameanza mazungumzo na kiungo wa Leicester City na Ubelgiji Youri Tielemans. Newcastle United na Barcelona pia wanavutiwa na mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 25. (Football Insider)


Chelsea wameanza mazungumzo na kiungo wa kati wa Ufaransa N'Golo Kante, 32, kuhusu kandarasi mpya. (Fabrizio Romano) Leicester City wanamfikiria meneja mlezi mwenye uzoefu, kama vile Martin O'Neill au Rafa Benitez, kuchukua nafasi ya Brendan Rodgers hadi mwisho wa msimu. (Independent)


Leicester wamemtaja Graham Potter, aliyetimuliwa Chelsea hivi majuzi, na meneja wa Brentford Thomas Frank kama walengwa wa majira ya joto, huku kocha wa zamani wa Southampton Ralph Hasenhuttl na Jesse Marsch, aliyewahi kuichezea Leeds, pia wakitajwa kuwa chini ya uangalizi. (Sky Sports)


Meneja wa zamani wa Borussia Monchengladbach Adi Hutter pia anaweza kuwa chaguo kwa Leicester. (mail) The Foxes wanaongoza katika mbio za kumsajili kipa wa Valencia na Georgia Giorgi Mamadashvili, 22. (Fabrizio Romano)


Burnley wanataka kumsajili winga wa Ajax na Uholanzi Sontje Hansen mwenye umri wa miaka 20 msimu huu wa joto. (Football Insider)


Arsenal wako kwenye mazungumzo na wawakilishi wa Reiss Nelson kuhusu kuongeza mkataba wa mshambuliaji huyo wa miaka 23 wa Uingereza. (Fabrizio Romano)


BBC



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz