Tetesi za usajili barani ulaya Leo Ijumaa - EDUSPORTSTZ

Latest

Tetesi za usajili barani ulaya Leo Ijumaa

Kupata Kifurushi cha bure Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Bayern Munich wana nia ya kumsajili mshambuliaji wa Uingereza Harry Kane, 29, kutoka Tottenham msimu huu wa joto, hata hivyo Manchester United wapo mstari wa mbele kumnyakua kwa sababu mchezaji huyo anataka kusalia katika Ligi ya Premia. (Mirror)


Lakini mabingwa wa Ujerumani Bayern wako tayari kujaribu kujitolea kwa Tottenham kumsaini nyota huyo kwa kutoa ofa kubwa kwa nahodha wa Uingereza Kane. (Independent)


Liverpool, Chelsea na Manchester United wana nia ya kumsajili kiungo wa kati wa Brighton na Argentina Alexis Mac Allister, 24, ambaye atafurahia uhamisho wa majira ya joto. (Guardian)


Real Madrid wako tayari kuwasilisha ombi jipya la kutaka kumsajili beki wa Uingereza Reece James, 23, iwapo Chelsea italazimika kuuza wachezaji msimu huu wa joto. (Mail)


Barcelona wanatarajia Chelsea kufanya jaribio jingine la kumsajili winga wa Rafinha, 26, msimu huu wa joto. (Sport - kwa Kihispania)


Aliyekuwa mkufunzi wa Bayern Munich Julian Nagelsmann, 35, amealikwa kukutana na bodi ya Chelsea huku klabu hiyo ikiendelea kutafuta meneja mpya wa kudumu.


Bosi wa zamani wa Uhispania Luis Enrique, 52, tayari amefanya mazungumzo na klabu hiyo (Bild - kwa Kijerumani)


Chelsea wana uhakika wa kufikia makubaliano na kiungo wa kati wa Uingereza , 24, kuhusu kandarasi mpya. (90min)


Manchester City na Chelsea zote zilituma maskauti kumtazama mlinzi wa Monaco Mfaransa Axel Disasi, 25, wikendi iliyopita. (Le Parisien - kwa Kifaransa)


Fulham wanafikiria kumnunua kiungo wa kati wa Porto wa Colombia Mateus Uribe, 32, kuichukua nafasi ya mchezaji wa kimataifa wa Ureno Joao Palhinha, 27, ambaye analengwa na Manchester United . (Sun)


Kiungo wa kati wa Colombia James Rodriguez, 31, ni mchezaji huru baada ya kukubali kusitisha kandarasi yake katika klabu ya Olympiacos ya Ugiriki (Liverpool Echo)


Mshambuliaji wa Ufaransa Kylian Mbappe, 24, anasema lengo lake ni kushinda Ligi ya mabingwa akiwa na Paris St-Germain, licha ya kukaribia kuondoka katika klabu hiyo kwenda Real Madrid mwaka jana. (90min)


BBC



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz