Tetesi za usajili barani ulaya Leo Jumanne - EDUSPORTSTZ

Latest

Tetesi za usajili barani ulaya Leo Jumanne

Kupata Kifurushi cha bure Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Aston Villa wana nia kubwa ya kusiani mkataba na kiungo wa kati wa England Kalvin Phillips, 27, kutoka Manchester City. (Football Insider)


Kiungo wa nyuma - kushoto wa England Ben Chilwell, 26, yuko tayari kusiani mkataba mpya wa miaka minne katika klabu ya Chelsea. (Athletic - subscription required)


Baba yake Lionel Messi na wakala wake Jorge walikutana na Barcelona lakini hakuna pendekezo la uhamisho lililotolewa kwa ajili ya mshambuliaji huyo Muagerntina mwenye umri wa miaka 35. (Cadena Ser, via Mirror)


Winga wa Ujerumani Marco Reus, 33, yuko tayari kusaini mkataba mpya katika Borussia Dortmund – lakini mshahara wake utakatwa ili aendelee kubakia katika klabu hiyo . (Bild - in German)


West Ham wanamfuatilia kwa karibu mchezaji wa safu ya kati-nyuma Muingereza Wan-Bissaka, 25, wakiwa na mpango wa kumhamisha msimu ujao wa kiangazi. (Football Insider)


Arsenal wako wazi kumuuza mshambuliaji wa kikosi cha England cha vijana walio chini ya umri wa miaka Folarin Balogun katika msimu ujao. Kijana huyo wamwenye umri wa miaka 21 kwa sasa yuko katika klabu ya Reims kwa mkataba wa mkopo. (Times - subscription required)


Arsenal na Chelsea ni miongoni mwa klabu kadhaa zinazotaka kumvhukua kiungo wa kati – kulia wa Wolfsburg na Ujerumani Ridle Baku, 25. (Bild - in German)


Chelsea ina matumaini ya kuendela kuwa na Joao Felix msimu ujao. The Blues walisaini mkataba wa mkopo na mshambuliaji huyu Mreno mwenye umri wa miaka 23 kutoka klabu ya Atletico Madrid mwezi Januari. (Fabrizio Romano)


Newcastle United inataka kusiani mkataba na mshambuliaji Mbrazili Joao Pedro, 21, kutoka Watford katika msimu ujao wa kianagazi. (Football Insider)


Brighton wana matumaini ya kuafikia mkataba mpya na kiuongo wa safu ya mashambulizi wa Jamuhuri ya mwenye umri wa miaka 18 Evan Ferguson, licha Manchester United na Tottenham kuwa na nia naye. (Mail)


BBC



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz