Rashford azua hofu man united - EDUSPORTSTZ

Latest

Rashford azua hofu man united

Kupata Kifurushi cha bure Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Mshambuliaji wa Manchester United, Marcus Rashford, huenda akaukosa mchezo wa Mkondo wakwanza wa Robo Fainali Ligi ya Europa dhidi ya Sevilla utakaochezwa keshokutwa Alhamis (April 13).


Taarifa zinaripoti kuwa Benchi la Ufundi la Manchester United linasubiri uhakika kutoka kwa madaktari kuhusu hali ya Mshambuliaji huyo aliye katika kiwango bora msimu huu 2022/23.


Rashford alipata maumivu ya misuli wakati wa mchezo wa Ligi Kuu England dhidi ya Everton, ambao ulishuhudia Mashetani Wekundu wakiibuka na ushindi wa mabao 2-0.


Inaaminika Rashford alikuwa akisumbuliwa na maumivu ya nyonga na huenda akakaa nje ya dimba kwa muda wa majuma matatu, lakini taarifa ya vipimo itaainisha kwa undani.


Michezo mingine ya Europa League Robo Fainali.


Juventus vs Sporting CP


Feyenoord vs Sevilla


Bayer Leverkusen vs Royale Union Saint-Gilloise




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz