Mwamuzi aliye mpiga kiwiko Robertson aingia matatani - EDUSPORTSTZ

Latest

Mwamuzi aliye mpiga kiwiko Robertson aingia matatani

Kupata Kifurushi cha bure Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 Beki wa kushoto wa Liverpool Andy Robertson alipigwa kiwiko na msaidizi wa mwamuzi Constantine Hatzidakis katika tukio la kushangaza mara tu baada ya filimbi ya mapumziko ya mechi ya Jumapili ya Ligi Kuu dhidi ya Arsenal


Nahodha wa Scotland alimwendea mwamuzi huyo msaidizi ambaye kisha akaweka kiwiko chake kwenye kidevu cha Robertson


Robertson alionyeshwa kadi ya njano na mwamuzi Paul Tierney huku akipinga kwa hasira


Arsenal waliongoza 2-1 hadi mapumziko, lakini Liverpool waliokoa sare ya 2-2 huku bao la kichwa la Roberto Firmino dakika ya 87 likizima nia ya vinara hao kutwaa taji hilo kwa mara ya kwanza tangu 2004.


Hatzidakis sasa anakabiliwa na uchunguzi kuhusu mwenendo wake baada ya bodi ya waamuzi ya PGMOL kusema itapitia tukio hilo


"PGMOL inafahamu kuhusu tukio lililohusisha mwamuzi msaidizi Constantine Hatzidakis na beki wa Liverpool Andrew Robertson wakati wa mapumziko wakati wa mechi ya Liverpool dhidi ya Arsenal kwenye uwanja wa Anfield. Tutapitia suala hilo kikamilifu," taarifa hiyo ilisema



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz