Matokeo Ihefu Fc vs Simba leo April 10 - EDUSPORTSTZ

Latest

Matokeo Ihefu Fc vs Simba leo April 10

Kupata Kifurushi cha bure Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Mkubwa ni mkubwa tu! Habari ndio hiyoooooo, Vijana wanasema Ihefu wamepasuka hapohapo sebuleni kwao!


Sio mwingine! Ni yuleyule Jean Baleke magoliiiii, amewalaza na viatu Ihefu Fc huko Mbarali, Mbeya


Mabao yake ya dakika za jioni yemetosha kuihakikishia Simba ushindi wa mabao 2-0 na kuzoa alama zote tatu


Kikosi cha Simba leo kimewapa somo mashabiki wake, ni muhimu kuwa na imani na timu yao


Lawama zilikuwa nyingi baada ya kocha Robertinho Oliveira kufanya mabadiliko makubwa ya kikosi chake akiwaacha nje nyota wake muhimu


Leo Robertinho ni mshindi na wale waliokuwa wakiponda uamuzi wake wanapaswa kutumia nguvu ileile kumpongeza


Baleke amewafunga Ihefu Fc mabao matano katika kipindi cha siku tatu


Huyu ni mwamba kwelikweli! Hawa Mbogo Maji hawatamsahau kamwe..!


Ni ushindi muhimu kwa Simba ambao unaongeza presha katika mbio za ubingwa sasa zikibaki alama tano tu



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz