Mechi ya Yanga dhidi ya Singida Big Stars yasogezwa mbele - EDUSPORTSTZ

Latest

Mechi ya Yanga dhidi ya Singida Big Stars yasogezwa mbele

Ofa ya Bando la Internet wiki BURE Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Bodi ya Ligi Kuu itaupangia tarehe nyingine mchezo wa ligi kuu kati ya Singida BS dhidi ya Yanga ambao ulipaswa kupigwa mwishoni mwa wiki


Yanga inatarajiwa kusafiri nchini Nigeria kwa ajili ya mchezo wa mkondo wa kwanza robo fainali kombe la Shirikisho barani Afrika dhidi ya Rivers United utakaopigwa Jumapili April 23


Mchezo wa marudiano utapigwa April 30 katika uwanja wa Benjamin Mkapa


Baada ya Singida BS, mchezo utakaofuata ni dhidi ya Dodoma Jiji ambao utapigwa uwanja wa Azam Complex, Chamazi


Ratiba ya mchezo huo nayo huenda ikaathiriwa kutokana na ratiba ta mechi za CAF


Yanga itakwenda kuhitimisha msimu mkoani Mbeya kwa mechi mbili dhidi ya Mbeya City na Tanzania Prisons


Katika mechi nne zilizosalia, Yanga inahitaji alama nane ili kitetea ubingwa kwa msimu wa pili mfululizo


Wananchi pia wanakabiliwa na mchezo wa nusu fainali kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) dhidi ya Singida BS ambao utapigwa uwanja wa Liti, Singida



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz