Matokeo Tp mazembe vs Yanga Leo Jumapili - EDUSPORTSTZ

Latest

Matokeo Tp mazembe vs Yanga Leo Jumapili

Kuingiza pesa Mtandaoni bure Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 
Yanga imefanikiwa kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya TP Mazembe katika mchezo wa kombe la Shirikisho uliopigwa uwanja wa TP Mazembe huko Lubumbashi, DR Congo


Bao la Farid Mussa lililopatikana kwenye kipindi cha pili lilitosha kuihakikishia Yanga ushindi huo muhimu ambao unaweza kuwahakikishia kumaliza vinara wa kundi D


Krosi ya Jesus Moloko ilimshinda mlinda lango wa Mazembe kabla ya kuangukia mguuni kwa Farid aliyeujaza mpira kimiani kwa mguu wake wa kulia


Ilikuwa mechi ngumu iliyopigwa katika uwanja wa nyasi bandia ambao kwa kiasi kikubwa uliwapa wakati mgumu wachezaji wa Yanga huku wenyeji wakitawala


Yanga imefikisha alama 13 wakati US Monastir wana alama 10 wakitarajiwa kucheza na Real Bamako saa 4 usiku


Ili kuishusha Yanga kileleni, Monastir watahitaji kushinda kuanzia mabao matatu




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz