Matchday Live: Simba vs Yanga Itazame Hapa - EDUSPORTSTZ

Latest

Matchday Live: Simba vs Yanga Itazame Hapa


 Baada ya tambo za takribani wiki nzima, mzizi wa fitna unakwenda kukatwa pale uwanja wa Benjamin Mkapa leowakati watani Simba na Yanga watakapoumana kwenye mchezo wa ligi kuu ya NBC


Mchezo huo una umuhimu wa kipekee kwa kila timu na pengine hiyo inaweza kuwa sababu ya kuongeza ushindani


Simba wakiwa wenyeji wa mchezo huo, itakuwa rasmi wameondoka katika mbio za ubingwa kama watapoteza


Ushindi kwao hautamaanisha wamerejea katika mbio za ubingwa kwa asilimia 100 pia kwani bado watakuwa na deni la alama tano dhidi ya Yanga


Ili waweze kuwa mabingwa watalazimika kuiombea Yanga mabaya katika mechi nne zitakazokuwa zimesalia huku wao wakitakiwa kushinda mechi zote


Kwa Yanga ushindi dhidi ya Simba leo utawapa uhakika wa kutetea ubingwa wao kwa msimu wa pili mfululizo


Kama Yanga itashinda leo, itahitaji alama mbili tu kutoka mechi nne zitakazokuwa zimesalia ili kurejesha ubingwa Jangwani kwa mara ya 29


Wakati Simba wakiwa na mabadiliko katika benchi lao la ufundi, Yanga wanakwenda kucheza dabi ya 9 wakiwa na Kocha Nasreddine Nabi


Takwimu zinaibeba Yanga katika mchezo huo kwani mara ya mwisho kupoteza mchezo wa ligi dhidi ya Simba ni miaka mitatu iliyopita


Nabi amekuwa mbabe wa dabi kwani katika mechi nane alizoiongoza Yanga, ameshinda nne, katoka sare tatu na kupoteza mchezo mmoja


Je leo ataendeleza ubabe wake dhidi ya Simba? Mtanange utapigwa kuanzia saa 11 jioni


Vita kubwa inatarajiwa kushuhudiwa kati ya washambuliaji Wacongoman Fiston Mayele wa Yanga na Jean Baleke wa Simba


Baleke amekuwa katika kiwango bora cha kupachika mabao, akifunga mabao saba katika mechi tano za ligi kuu alizocheza tangu alipojiunga na Simba


Hii itakuwa mechi yake ya kwanza ya derby lakini amebeba matumaini makubwa ya Wanasimba kutokana na form aliyonayo


Mayele ndiye kinara wa mabao katika ligi kuu, akifunga mabao 16. Hii itakuwa mechi yake ya saba ya derby akiwa amefunga mabao matatu katika mechi sita alizokutana na Simba


Safu ya ushambuliaji ya Simba inaonekana kuwa hatari zaidi baada ya ongezeko la Saido Ntibazonkiza ambaye anashirikiana vyema na Baleke na Clatous Chama kinara wa pasi za mabao


Hata hivyo Yanga wanajivunia ukuta imara wakiwa timu iliyoruhusu mabao machache zaidi kwenye ligi msimu huu


Yanga wameonyesha wana uwezo wa kulinda ushindi hata wa bao moja kwa dakika 90 lakini ni tofauti kwa watani zao Simba


Katika mechi mbili zilizopita kwenye derby, Simba ilitangulia kufunga lakini ikapoteza moja na kutoka sare moja baada ya dakika 90


Matumaini ya mashabiki ni kuwa watashuhudia mechi nzuri yenye ushindani wa aina yake siku ya leo

Mechi Itakuwa LIVE kwenye App yetu bofya hapa kuidownload sasa ili uweze kuitazama mechi hii kupitia simu Yako



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz