LIVE : WYDAD ATHLETIC VS SIMBA Itazame hapa - EDUSPORTSTZ

Latest

LIVE : WYDAD ATHLETIC VS SIMBA Itazame hapa

 

Leo 'kitaeleweka' nchini Morocco wakati Wekundu wa Msimbiazi Simba Sc watakaposhuka uwanja wa Mohammed V kuwakabili wenyeji wao Wydad Athletic katika mchezo wa mkondo wa pili robo fainali ya michuano ya ligi ya mabingwa barani Afrika


Hakuna unyonge kwa Simba kuelekea mchezo huo, baada ya kuishia hatua ya robo fainali mara nne, wakati huu Wanasimba wanasema HAPANA, nusu fainali itawezekana


Kocha Mkuu wa Simba Robertinho Oliveira amesema kikosi chake kiko tayari kwa mchezo, ari na morali ya wachezaji wake iko juu, dhamira ni kushinda au kupata matokeo chanya ambayo yataipeleka Simba nusu fainali


Kumekuwa na sintofahamu kuhusu muda wa mchezo lakini sasa ni rasmi mchezo huo utapigwa saa 2 usiku kwa saa za Morocco, kwa muda wa Tanzania ni saa 4 usiku


Ni mechi ngumu lakini kwa hatua ambayo Simba imefika, haipaswi kuhofia kukabiliana na mpinzani aina ya Wydad kwani kwa sasa Simba iko kwenye daraja moja nao kwa kuangalia viwango vya ubora CAF


Simba inaongoza kwa bao 1-0 kutoka ushindi wa mechi ya mkondo wa kwanza, inawezekana kupata ushindi katika mechi ya marudiano leo

Mechi itakuwa live kwenye app yetu bofya hapa kuidownload app sasa ili uweze kuitazama mechi hii live kupipitia simu yako



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz