Hii hapa taarifa Rasmi kuhusu majeraha Kapombe na Kibu Dennis - EDUSPORTSTZ

Latest

Hii hapa taarifa Rasmi kuhusu majeraha Kapombe na Kibu Dennis

Kuingiza pesa Mtandaoni bure Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Klabu ya Simba imebainisha kuwa wachezaji Shomari Kapombe na Kibu Denis ambao walipata majeraha kwenye mchezo wa kuhitimisha hatua ya makundi ya michuano ya ligi ya mabingwa dhidi ya Raja Casablanca, watafanyiwa vipimo kubaini ukubwa wa majeraha yao leo


Kapombe na Kibu walishindwa kumaliza dakika zote tisini katika mchezo uliopigwa huko Morocco usiku wa kuamkia Jumamosi na Simba kupoteza kwa mabao 3-1


Hata hivyo Daktari wa Simba Edwin Kagalo amewatoa hofu Wanamsimbazi kuwa uchunguzi wa awali wa majeraha ya Kapombe hayakuonekana kuwa makubwa hivyo beki huyo mahiri wa upande wa kulia anaweza kupewa mapumziko ya siku chache


Nyota mwingine ambaye atafanyiwa vipimo ni winga Peter Banda aliyepata majeraha wakati akiwa kwenye majukumu ya timu ya Taifa


Msimu huu haukuwa mzuri kwa Banda kwani majeraha yamekuwa changamoto kubwa kwake



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz