Azam Fc dimbani Leo dhidi ya Mtibwa sugar Robo fainali FA - EDUSPORTSTZ

Latest

Azam Fc dimbani Leo dhidi ya Mtibwa sugar Robo fainali FA

Kuingiza pesa Mtandaoni bure Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

Licha ya kuyumba kidogo tofauti na walivyoanza msimu huu kwenye ligi kuu, Azam Fc leo wana nafasi ya kufanya vizuri katika mchezo wa robo fainali kombe la Shirikisho la Azam (ASFC) dhidi ya Mtibwa Sugar


Mchezo huo utapigwa katika uwanja wa Azam Complex, Chamazi saa 1 usiku


Kwa Azam Fc kombe la FA sasa ni muhimu zaidi kwao ili kujihakikishia kushiriki michuano ya CAF msimu ujao


Kwenye Ligi Kuu wanashika nafasi ya nne nyuma ya Yanga, Simba na Singida Big Stars


Msimu ujao Tanzania itatoa timu nne kwenye michuano ya CAF ambapo mshindi wa kwanza na pili katika ligi kuu watacheza ligi ya mabingwa wakati mshindi wa tatu na bingwa wa kombe la FA watacheza kombe la Shirikisho


Kama itatokea bingwa wa FA ni timu iliyomaliza nafasi ya kwanza au pili kwenye ligi kuu, timu itakayoshika nafasi ya nne kwenye ligi itakwenda Shirikisho


Azam Fc wanakutana na Mtibwa Sugar ambayo msimu huu imekuwa haitabiriki. Timu hizo zilipokutana kwenye ligi uwanja wa Manungu, Azam Fc iliibuka na ushindi wa mabao 4-3


Baada ya mechi ya FA, timu hizo zitachuana tena katika mchezo wa ligi kuu utakaopigwa hapohapo kwenye uwanja wa Azam Complex, April 15



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz