Singida Big Stars yajipanga kumng'oa Kakolanya Simba - EDUSPORTSTZ

Latest

Singida Big Stars yajipanga kumng'oa Kakolanya Simba

Kuingiza pesa Mtandaoni bure Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Kikosi cha Singida Big Stars kinaendelea kujifua jijini Dodoma tayari kwa pambano lijalo la robo fainali kombe la FA dhidi ya Mbeya City litakalopigwa mjini Singida


Singida BS jana walicheza mechi ya kirafiki dhidi ya Dodoma Jiji na kuibuka na ushindi wa mabao 2-1 katika uwanja wa Jamhuri


Za ndani ni kuwa mabosi wa timu hiyo wameanza mipango ya kumng'oa kipa wa Simba Beno Kakolanya


Singida BS wameanza mazungumzo na kipa huyo ambaye mkataba wake unaelekea mwishoni kwa lengo la kumsajili aitumie kuanzia msimu ujao.


Mkataba wa Kakolanya na Simba unaisha mwishoni mwa msimu huu na hadi sasa inadaiwa hakuna makubaliano ya kusaini dili jipya licha ya mabosi wa Msimbazi kuzungumza naye hivi karibuni, hivyo kutoa nafasi kwa kipa huyo namba mbili ndani ya timu hiyo kutafuta changamoto mpya.


Singida BS wamekuwa na changamoto katika eneo lao la magolikipa sasa wakimtegemea Benedict Haule baada ya kumtoa kwa mkopo Metacha Mnata kunako klabu ya Yanga



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz