Rais Samia aongeza tiketi 7000 Stars vs Uganda - EDUSPORTSTZ

Latest

Rais Samia aongeza tiketi 7000 Stars vs Uganda

Kuingiza pesa Mtandaoni bure Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA


 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Dkt. Samia Suluhu Hassan amenunua tiketi nyingine 7,000 baada ya awali kununua tiketi 2,000 wakati wa hamasa iliyoongozwa na Afisa Habari wa TFF, Clifford Ndimbo akishirikiana na Maafisa Habari wa Azam FC, Simba na Yanga.


Waziri Mkuu Mh Kassim Majaliwa pia ameongeza tiketi nyingine 2,000 huku wadau wengine wa Wizara mbalimbali wakichangia tiketi 11,000 na sasa kufikia jumla ya tiketi 20,000.


Wizara ya Sanaa, Utamaduni na Michezo kupitia kwa Katibu wake Mkuu, Saidi Yakubu amemkabidhi Rais wa TFF, Wallace Karia kwa ajili ya kufanya utaratibu wa kuzigawa tiketi hizo zilizopatikana


Tanzania na Uganda zitachuana siku ya Jumanne, March 28 katika uwanja wa Benjamin Mkapa, kwenye mchezo wa kuwania kufuzu michuano Afcon 2023



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz