Moloko awahaidi Jambo hili mashabiki wa Yanga - EDUSPORTSTZ

Latest

Moloko awahaidi Jambo hili mashabiki wa Yanga


 Kuingiza pesa Mtandaoni bure Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA

Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

Winga machachari wa Yanga Jesus Moloko amewataka mashabiki kuchangamkia fursa ya kusafiri na timu DR Congo kwa ajili ya mchezo wa kuhitimisha hatua ya makundi kombe la Shirikisho dhidi ya TP Mazembe


Mchezo huo utapigwa April 02 katika dimba la TP Mazembe jiji la Lubumbashi, Yanga kihitaji kushinda ili kujiweka katika nafasi nzuri ya kumaliza kinara wa kundi D


Moloko amesema wachezaji wangependa kuona lile 'vibe' la mashabiki katika dimba la Mkapa likihamia Lubumbashi


"Ujumbe wangu kwa mashabiki wa Yanga waje kwa wingi twende Congo. Sisi wachezaji tuko tayari na tunawaahidi tutakwenda kupambana kuhakikisha tunapata ushindi," alisema Moloko


Kwa Moloko haitakuwa mara yake ya kwanza kucheza kunako dimba la TP Mazembe kwani kabla ya kutua Yanga aliitumikia AS Vita


Yanga itasafiri DR Congo ikiwa na faida ya wachezaji sita ambao waliwahi kuitumikia AS Vita


Tuisila Kisinda, Fiston Mayele, Djuma Shaban, Joyce Lomalisa na Yannick Bangala hawatakuwa wageni katika uwanja wa TP Mazembe



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz