Mohammed Dewji 'Mo' awapongeza Yanga Kwa hili - EDUSPORTSTZ

Latest

Mohammed Dewji 'Mo' awapongeza Yanga Kwa hili

Kuingiza pesa Mtandaoni bure Bonyeza HAPA


Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA


Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA

 

Mwekezaji wa klabu ya Simba Bilionea Mohammed Dewji 'Mo' amesema bado ndoto yake kubwa ni kuiona Simba ikitwaa taji la ligi ya mabingwa barani Afrika


Mo ambaye tangu aanze kuwekeza Simba, katika kipindi chake cha miaka mitano, Simba imefanikiwa kutinga robo fainali ya michuano ya CAF mara nne


Simba imecheza robo fainali ya ligi ya mabingwa mara tatu na kombe la Shirikisho mara moja


Mo amesema Simba tayari ina mataji 22 ya ligi kuu, hivyo angependa zaidi kutwaa taji la Ligi ya Mabingwa


Aidha Mo ameeleza kufurahia na ushindani ulioletwa na Yanga kwenye ligi ya ndani akiamini hiyo ni chachu kwao kujiimarisha na kuifanya ligi kuwa bora zaidi


"Nawapongeza Yanga kuleta ushindani mkubwa ndani ya Ligi wamefanya kazi kubwa, mpira usipokuwa na ushindani hauna ladha kwa hilo lazma niwapongeze Yanga na nawatakia kila La kheri kwenye mashindano Confederation na wao pia wafanikiwe ili timu nne ziendelee kushiriki kwenye mashinda haya makubwa"


"Mimi naona sisi (Simba) lazima tujipange upya ili tuweze sio tu kwenye Ligi. Huku kwenye ligi tumeshashinda mara 22 kwangu ni muhimu zaidi kushinda Champions League Africa," alisema Mo katika mahojiano na Global TV Online




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz