Mezul Ozil astaafu soka la kulipwa - EDUSPORTSTZ

Latest

Mezul Ozil astaafu soka la kulipwa

Kuingiza pesa Mtandaoni bure Bonyeza HAPA

Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA

Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA
 
Kiungo wa zamani wa Arsenal, Real Madrid na timu ya Taifa ya Ujerumani Mezut Azi ametangaza kustaafu rasmi kutoka kwa soka ya kulipwa akiwa na umri wa miaka 34 siku ya Jumatano.

Ozil ametoa taarifa rasmi kwa vyombo vya habari juu ya uamuzi wake wa kuachana na soka la kulipwa

"Baada ya kufikiria kwa uangalifu, ninatangaza kustaafu mara moja kutoka kwa kandanda ya kulipwa. Nimekuwa na fursa ya kuwa mchezaji wa soka wa kulipwa kwa karibu miaka 17 sasa nahisi safari hii imefika mwisho"

"Katika wiki na miezi ya hivi karibuni, nimekabiliwa na changamoto za majeraha, nadhani ni wakati wa kuondoka kwenye hatua kubwa ya soka," Ozil alisema katika taarifa yake.

"Imekuwa safari ya ajabu iliyojaa nyakati na hisia zisizosahaulika. Nataka kushukuru vilabu vyangu - Schalke, Werder Bremen, Real Madrid, Arsenal FC, Fenerbahce, Basaksehir na makocha walioniunga mkono, pamoja na wachezaji wenzangu ambao wamekuwa marafiki"

"Shukrani za pekee lazima ziende kwa wanafamilia yangu na marafiki zangu wa karibu. Wamekuwa sehemu ya safari yangu tangu siku ya kwanza na wamenipa upendo na usaidizi mwingi, kupitia nyakati nzuri na mbaya. Asante kwa mashabiki wangu wote ambao wamenionyesha upendo mwingi bila kujali mazingira na bila kujali nilikuwa nikiwakilisha klabu gani"

"Sasa ninatazama kila kitu kilicho mbele yangu pamoja na mke wangu mrembo, Amine, na binti zangu wawili warembo, Eda na El"

Ozil aliichezea Ujerumani mechi 92, alishinda Kombe la Dunia akiwa na taifa hilo mwaka 2014. Alicheza katika vilabu kama Real Madrid na Arsenal, kabla ya kuhamia Fenerbahce. Alimaliza soka lake katika klabu ya Uturuki, Istanbul Basaksehir



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz