Mbappe aulamba apewa majukumu Mapya - EDUSPORTSTZ

Latest

Mbappe aulamba apewa majukumu Mapya

Kuingiza pesa Mtandaoni bure Bonyeza HAPA

Ajira Mpya zilizotangazwa leo Bonyeza HAPA

Msimamo wa ligi kuu Tanzania Bonyaza HAPA
 
Kylian Mbappe atachukua nafasi ya nahodha wa Ufaransa baada ya Hugo Lloris kujiuzulu kufuatia kushindwa kwa fainali ya Kombe la Dunia dhidi ya Argentina, chanzo cha karibu cha timu hiyo kimeiambia AFP.


Mshambulizi wa Paris Saint-Germain Mbappe, 24, amekubali jukumu hilo baada ya mazungumzo na kocha Didier Deschamps


Mchezo wake wa kwanza kama nahodha utakuwa wa Ijumaa wa kufuzu kwa Euro 2024 dhidi ya Uholanzi Uwanja wa Stade de France


Itakuwa mechi ya kwanza ya Les Bleus tangu kushindwa kwenye fainali ya Kombe la Dunia huko Doha mnamo Desemba 18.


Kipa wa Tottenham Lloris, 36, alimaliza soka lake la kimataifa mwezi Januari, wiki chache baada ya Argentina kuwashinda Wafaransa hao kwa mikwaju ya penalti kufuatia mechi ya kusisimua iliyoisha 3-3 katika muda wa ziada.


Lloris alikuwa nahodha kwa zaidi ya muongo mmoja. Mshambulizi wa Atletico Madrid Antoine Griezmann alitangazwa kuwa makamu wa nahodha baada ya beki wa kati wa Manchester United Raphael Varane pia kutundika daruga zake kufuatia kushindwa na Argentina mwezi Desemba.


Mbappe, ambaye alifunga hat-trick kwenye fainali ya Kombe la Dunia, alikuwa akihusishwa pakubwa na nafasi ya unahodha kwa wiki kadhaa



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz