WAFAHAMU Al Hilal Wapinzani wa Yanga CAF Champions League 2022/2023 - EDUSPORTSTZ

Latest

WAFAHAMU Al Hilal Wapinzani wa Yanga CAF Champions League 2022/2023

WAFAHAMU Al Hilal Wapinzani wa Yanga CAF Champions League 2022/2023

WAFAHAMU Al Hilal Wapinzani wa Yanga CAF Champions League 2022/2023

Yanga vs Al Hilal CAF Champions League 2022/23 ,Young Africans vs Al Hilal, Young Africans vs AL-Hilal, Yanga vs Al-Hilal CAF Champions League, Yanga vs Al Hilal CAF, Al Hilal vs Yanga, Al Hilal wapinzani wa Yanga, Ifahamu Al Hilal wapinzani wa Yanga CAF Champions League 2022/2023.

WAFAHAMU Al Hilal Wapinzani wa Yanga CAF Champions League 2022/2023

AL Hilal wapinzani wa Yanga CAF

KLABU ya Al Hilal (Kiarabu: نادي الهلال للتربية), inayojulikana kama Al Hilal Omdurman au kwa urahisi Al Hilal, ni klabu ya soka ya Sudan yenye makao yake Makuu Mjini Omdurman ambayo inashiriki Ligi Kuu ya Sudan.

Al Hilāl ni neno la Kiarabu linalomaanisha mpevu – Jina lililochaguliwa usiku ambapo mpevu wa mwezi ulionekana katika Omdurman.Pia ni klabu ya kwanza Duniani kupewa jina (AL- HILAL).

Hawa ndio Wafalme wa Soka la Sudan, Ndio klabu iliyobeba Mataji mengi zaidi nchini humo na ndio Wawakilishi bora zaidi wa CECAFA kwenye CAF.

Al Hilal imeshacheza Fainali za CAF mara 2 zote Ikipoteza, Ilikua 1987 dhidi ya Al Ahly SC ya Misri na 1992 dhidi ya Wydad Casablanca ya Morocco.

Al Hilal Imecheza Nusu Fainali ya Michuano ya CAF Champions League mara nyingi zaidi ya klabu yoyote ya CECAFA, ikifanya hivyo mara 5 na Robo Fainali nyingi, imecheza makundi mara mwisho msimu jana wa 2021/2022.

WAFAHAMU Al Hilal Wapinzani wa Yanga CAF Champions League 2022/2023

Al Hilal

Al Hilal ina kikosi kinachokaririwa kuwa na thamani ya Dola za Kimarekani $ Million 2.75 zaidi ya Tsh Bilioni 6.3.Yanga vs Al Hilal CAF Champions League 2022/23 ,Young Africans vs Al Hilal, Young Africans vs AL-Hilal, Yanga vs Al-Hilal CAF Champions League, Yanga vs Al Hilal CAF, Al Hilal vs Yanga, Al Hilal wapinzani wa Yanga, Ifahamu Al Hilal wapinzani wa Yanga CAF Champions League 2022/2023.

Baada ya misimu kadhaa kutofanya makubwa kimataifa, Hilal walimuomba Tycoon, Bilionea Turk El Sheikh wa Saudia Arabia kuwa raisi wa heshima wa klabu hiyo, huyu ndiye aliyeinunua Pyramid FC ya Misri kutoka Al Assiyout kitaka kuifanya klabu hatari zaidi Misri na Afrika na baadae akaiuza.

Mwamba huyu anayemiliki Klabu ya Almeria ya Hispania aliweka mzigo wa kutosha kwa kuongeza nyota wenye uwezo ili Hilal ifanye vizuri zaidi Afrika.

Aliingia Msimu uliopita ila msimu huu akaweka Pesa ambayo kmenunua nyota wengi kama Issa Fofana kutoka San Pedro ya Ivory Coast, Cloud Singone kutoka Asec Mimosas ya Ivory Coast pia Imoro Ibrahim kutoka Asante Kotoko ya Ghana, John Mano (aliyewafunga Simba mechi ya Kirafiki Kirafiki), Makabi Lilepo kutoka DR Congo na Lamine Diedhou kutoka Senegal.

Kutokana udhamini huo Al Hilal wakafanikiwa kumrejesha Mshambuliaji wao hatari (mtambo wao wa mabao) Waleed Bkhet aliyesajiliwa Kuwait akitoke Hilal na sasa amerejea tena.

Kama haitoshi wakamsajili Kocha mwenye taji la Shirikisho Afrika Msimu Jana Frolent Ibenge raia wa DRC na mpango wao wa sasa ni kufika nusu Fainali ya CAF Champions League.

WAFAHAMU Al Hilal Wapinzani wa Yanga CAF Champions League 2022/2023

Fiston Kalala Mayele Yanga SC

Young Africans Sports Club, ambayo wakati mwingine hujulikana kama Yanga, ni klabu ya soka ya Tanzania inayocheza michezo yake ya nyumbani kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa Jijini Dar es Salaam na Makazi yake yapo Mtaa wa Jangwani, Dar es Salaam.

Klabu hiyo ilianzishwa mwaka 1935, na Uwanja wa Benjamin Mkapa ndio wanacheza michezo yao ya nyumbani. Jina la utani la klabu hiyo ni “Yanga,” na imeshinda mataji 28 ya Ligi Kuu na Mashindano kadhaa ya vikombe vya nyumbani.

Zaidi ya hayo, wameshiriki katika Mashindano mengi ya Ligi ya Mabingwa ya CAF na ni Mabingwa mara 5 wa michuano ya Klabu Bingwa Afrika Mashariki CECAFA.

Klabu hiyo ilikuja kuwakilisha harakati za kupinga ukoloni na maadili yake. Kundi la kisiasa la TANU lilihamasishwa kuchagua rangi ya manjano na kijani kibichi kama rangi zao kuu baada ya kuhusishwa na vijana wa Kiafrika ambao walishirikiana na wazalendo na wapigania uhuru.

Klabu hiyo sasa inapitia utaratibu utakaodumisha mfumo wa umiliki wa klabu kwa asilimia 49 kwa wawekezaji na asilimia 51 kwa wanachama wa klabu.

Klabu hiyo ina msuguano wa muda mrefu na wapinzani wake kutoka upande wa pili wa Jiji, Simba ambao wanachuana nao katika mchezo wa derby wa Dar es Salaam (wakati mwingine huitwa Kariakoo).

Shindano hilo lilishika nafasi ya tano kwenye Orodha ya Michezo maarufu zaidi ambayo hufanyika Barani Afrika.

Klabu ya Yanga SC ilianzishwa mwaka 1935, na Uwanja wa Benjamin Mkapa ndio Uwanja wao wa nyumbani na michezo yao ya nyumbani wanatumia Uwanja huo unaobeba watu 60,000.

KAA TAARIFA ZAIDI SOMA HAPA

PARMATCH Kumwaga Mamilioni kwa Wateja Wapya | Jisajili hapa Kushinda Zawadi

PARMATCH Kumwaga Mamilioni kwa Wateja Wapya

BETI NA PARMATCH USHINDE MAMILIONI

Kampuni ya Michezo ya KUBETI na KASINO za Mtandaoni Tanzania PARMATCH imezindua Ofa mpya ya Bonasi kwa Wateja wapya.

Kila mteja mpya atakayejisajili na PARMATCH atajinyakulia BONASI sawa na kiasi alichoweka kwa mara ya kwanza kuanzia Shilingi 1,000 hadi milioni moja kwa kila mteja.

Akizungumza katika uzinduzi wa BONASI hiyo Afisa Masoko wa Parmatch amesema kuwa Bonasi hiyo itawahusu wateja wapya watakaojisajili na kuweka salio kwenye akaunti zao.

Ili uweze kujisajili na PARMATCH unatakiwa kutembelea tovuti yao kwa kugusa HAPA Kisha Jisajili.

Kujiunga na PARMATCH na kupata Bonasi ya hadi 1,000,000 (Milioni Moja) Ukideposit salio kwenye akaunti yako Bofya HAPA.

Unaweza kupata Taarifa hii kwa undani zaidi kwa kubofya Parmatch.co.tz

The post WAFAHAMU Al Hilal Wapinzani wa Yanga CAF Champions League 2022/2023 appeared first on Nijuze Mpya -| Pata Habari zote za Michezo kitaifa na Kimataifa, Tetesi na Usajili, Magazeti ya Michezo, Ratiba na Matokeo, Mahusiano Pamoja na Nafasi za Kazi.



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz