SIMBA Queens Mabingwa CECAFA 2022, Rais Samia awapongeza - EDUSPORTSTZ

Latest

SIMBA Queens Mabingwa CECAFA 2022, Rais Samia awapongeza

SIMBA Queens Mabingwa CECAFA 2022, Rais Samia awapongeza

SIMBA Queens Mabingwa CECAFA 2022, Rais Samia awapongeza

SIMBA Queens Mabingwa CECAFA 2022, Rais Samia awapongezaTimu ya Simba Queens imetawazwa Mabingwa Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati CECAFA (SAMIA CUP 2022) baada ya kuibuka na ushindi wa bao 1-0 dhidi ya SHE Corporates ya Uganda, Mchezo wa Fainali uliofanyika kwenye wa Uwanja wa Azam Complex.

Mchezo ulikuwa mkali na wa kuvutia kutokana na timu zote kufahamiana vizuri kwani zilishakutana katika hatua ya makundi na Simba kuibuka na ushindi wa mabao 2-0.SIMBA Queens Mabingwa CECAFA 2022, Rais Samia awapongeza

Mlinda mlango wa SHE Corporates alionyesha kiwango bora katika mchezo huo kwa kuokoa michomo ya washambuliaji wa Simba ambapo kama si ubora wake basi Mabingwa hao wa Uganda wangefungwa mabao zaidi ya moja walilofungwa.SIMBA Queens Mabingwa CECAFA 2022, Rais Samia awapongeza

Kiungo mkabaji Vivian Corazone ndiye aliyeipatia Simba Qeeens bao pekee la ushindi kwa mkwaju wa penati dakika ya 47 ambalo liliihakikishia Simba kubakisha taji hilo katika ardhi ya nyumbani.SIMBA Queens Mabingwa CECAFA 2022, Rais Samia awapongeza

Ubingwa huu unaifanya Simba kupata tiketi ya kuuwakilisha Ukanda wa CECAFA katika Ligi ya Mabingwa Afrika na inakuwa timu ya kwanza kutoka Tanzania kufanya hivyo.

SIMBA Queens Mabingwa CECAFA 2022, Rais Samia awapongezaBaada ya kutwaa Ubingwa huo wa Ukanda wa Afrika Mashariki na Kati (CECAFA), Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mh. Samia Suluhu Hassan aliipongeza timu ya Simba Queens.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, Rais Samia alituma salamu za pongezi na kuitakia heri katika Michuano ya Ligi ya Mabingwa Afrika kwa Wanawake itakayofanyika nchini Morocco.

“Nawapongeza wanangu wa Simba Queens kwa ubingwa wa Afrika Mashariki na Kati (CECAFA) kwa Wanawake (SAMIA CUP). Mmejenga heshima kwa soka la Tanzania na nchi kwa ujumla.SIMBA Queens Mabingwa CECAFA 2022, Rais Samia awapongeza

“Nawatakia kheri katika Ligi ya Mabingwa Afrika (2022 CAF Women’s Champions League) itakayofanyika nchini Morocco,” ameandika Rais Samia.

Mchezaji wa Simba Queens, Aquino Corazone ndiye aliyeibuka mchezaji Bora wa Michuano ya CECAFA 2022.Aquino Corazone Simba Queens

 

 Golikipa Simba Queens Gelwa Yona, ndiye Golikipa Bora wa michuano ya CECAFA.Gelwa Yona Simba Queens

The post SIMBA Queens Mabingwa CECAFA 2022, Rais Samia awapongeza appeared first on Nijuze Mpya -| Pata Habari zote za Michezo kitaifa na Kimataifa, Tetesi na Usajili, Magazeti ya Michezo, Ratiba na Matokeo, Mahusiano Pamoja na Nafasi za Kazi.



Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz