DOGO WA YANGA B APIGA HAT-TRICK MICHUANO YA U20-Michezoni leo - EDUSPORTSTZ

Latest

DOGO WA YANGA B APIGA HAT-TRICK MICHUANO YA U20-Michezoni leo

Pakua App ya 'EDUSPORTSTZ NEWS' Uweze kufurahia Habari zote za Mapenzi; Udaku, Ajira na Michezo kila siku Ipo Google Playstore, Kwa Ku BONYEZA INSTALL Ili KUIDOWNLOAD Kwenye Simu yako nakutasoma habari zote hata kama hauna MB

MSHAMBULIAJI chipukizi wa Yanga, Clement Francis Mziza amekuwa mchezaji wa kwanza kupiga hat-trick kwenye Ligi ya Vijana chini ya umri wa miaka 20.
Nyota huyo alifunga mabao yote matatu akiisaidia timu yake kushinda 3-1 dhidi ya Geita Gold katika mchezo wao wa kwanza wa Kundi D usiku wa jana Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam.
Mechi nyingine ya Kundi D jana, KMC ilitoa sare y 1-1 na Kagera Sugar, wakati Kundi B, Mbeya Kwanza iliichapa 3-1 Ruvu Shooting na mabingwa watetezi, Mtibwa Sugar wakaitandika 4-0 Dodoma Jiji.
Michuano hiyo ilianza juzi, Kundi A; Biashara United ikitoka sare ya 0-0 na Namungo FC na Simba SC ikaichapa Polisi Tanzania 2-1, wakati Kundi C, Tanzania Prisons iliichapa Coastal Union 1-0 na wenyeji, Azam FC wakaichapa Mbeya City 3-2.




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz