ANCELOTTI AIPA REAL MADRID TAJI LA LA LIGA -Michezoni leo - EDUSPORTSTZ

Latest

ANCELOTTI AIPA REAL MADRID TAJI LA LA LIGA -Michezoni leo

Pakua App ya 'EDUSPORTSTZ NEWS' Uweze kufurahia Habari zote za Mapenzi; Udaku, Ajira na Michezo kila siku Ipo Google Playstore, Kwa Ku BONYEZA INSTALL Ili KUIDOWNLOAD Kwenye Simu yako nakutasoma habari zote hata kama hauna MB

KOCHA mkongwe Mtaliano, Carlo Ancelotti ameweka rekodi ya kushinda mataji ya ligi zote kubwa Ulaya baada ya jana kuiwezesha Real Madrid kutwaa ubingwa wa La Liga nchini Hispania.
Real Madrid imejihakikishia taji la La Liga msimu huu baada ya ushindi wa 4-0 dhidi ya Espanyol jana Uwanja Santiago Bernabéu Jijini Madrid, mabao ya Rodrygo dakika ya 33 na 43, Asensio dakika ya 55 na Karim Benzema dakika ya 81, hivyo kufikisha pointi 81 katika mchezo wa 34, ambazo haziwezi kufikiwa na wapinzani.
Ancellotti anabeba taji la La Liga baada ya awali kushinda mataji ya Ligi za nyumbani kwao, Italia, England, Ufaransa na Ujerumani hivyo kuwa kocha wa kwanza kubeba mataji ya ligi tano kubwa Ulaya.




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz