Tanzania Yatajwa Katika Nafasi ya 9 Kati ya nchi 10 Afrika zenye Barabara Bora - EDUSPORTSTZ

Latest

Tanzania Yatajwa Katika Nafasi ya 9 Kati ya nchi 10 Afrika zenye Barabara Bora


Mtandao wa Briefly.com umeitaja Tanzania katka nafasi ya 9 kati ya nchi 10 Afrika zenye barabara bora kwa mwaka 2021/2022. Ukanda wa Afrika Kaskazini umetoa nchi tatu (Egypt, Morocco &Algeria), Afrika Mashariki imetoa nchi tatu (Tanzania, Kenya &Rwanda). Hakuna nchi yoyote kutoka ukanda wa Afrika ya kati na ni nchi moja tu (Senegal) kutoka Afrka Magharibi iliyoingia kwenye orodha hiyo.

Ethiopia ambayo ina mtandao mkubwa wa barabara pamoja na "flyover" nyingi imeondolewa katika orodha hiyo licha ya mwaka jana kushika nafasi ya 7, kwa madai kuwa barabara zake japo ni nyingi na za kisasa lakini hazina ubora na huharibika baada ya muda mfupi.

Nini maoni yako? Kwa kadri unavyozifahamu barabara za nchi yetu, unadhani tumestahili kuingia top ten au tumebebwa?




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz