MABINGWA watetezi, Manchester City wameibamiza Brighton & Hove Albion mabao 3-0 katika mchezo wa Ligi Kuu ya England usiku wa Jumatano Uwanja wa Etihad Jijini Manchester.
Mabao ya Man City yamefungwa na Riyad Mahrez dakika ya 53, Phil Foden dakika ya 65 nw Bernardo Silva dakika ya 82.
Kwa ushindi huo, Man City inafikisha pointi 77 na kuendelea kuongoza ligi kwa pointi moja zaidi ya Liverpool baada ya wote kucheza mechi 32 na Brighton inabaki na pointi zake 40 za mechi 33 nafasi ya 10.
No comments:
Post a Comment