Elon Musk ataka Putin aje kwenye pambano ili mshindi aamue hatima ya Ukraine - EDUSPORTSTZ

Latest

Elon Musk ataka Putin aje kwenye pambano ili mshindi aamue hatima ya Ukraine



Katika hatua nyingine ya kushangaza, bilionea wa teknolojia wa Marekani Elon Musk anaonekana kumthubutu rais wa Urusi Vladimir Putin kwenye pambano la ana kwa ana, akipendekeza mshindi aamue hatima ya Ukraine.

Wanasiasa wa Ukraine hadi sasa wamekaribisha ofa hiyo, ambayo imetolewa kwa njia ya kukejeli.Meya wa Kyiv Vitali Klitschko, ambaye pia ni bondia wa zamani, alijibu kwa emoji tatu kali za mkono.

Rais wa Urusi bado hajajibu. Musk amekuwa mfuasi mkubwa wa Ukraine wakati wote wa uvamizi huo.

Mapema mwezi huu moja ya kampuni zinazomilikiwa na mfanyabiashara huyo wa teknolojia mwenye makao yake huko California, Starlink, ilisambaza Ukraine na idadi ya vyombo vya satelaiti vilivyokusudiwa kulinda ufikiaji wa mtandao nchini




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz