Siri 5 Ambazo Mke Hafai Kumwambia Mume wake Licha ya Utamu wa Penzi lao - EDUSPORTSTZ

Latest

Siri 5 Ambazo Mke Hafai Kumwambia Mume wake Licha ya Utamu wa Penzi lao


Yafuatayo ni mambo 5 ambayo mwanamke hapaswi kumwambia mume wake:

1. Idadi ya wanaume uliojamiiana nao kabla ya kuoana na mume wako

Hupaswi kumfahamisha mpenzi wako wa kiume au mume wako ni wanaume wangapi ulikutana nao kimwili kabla ya kuishi naye.


Sababu ni kwamba unaweza kufikiri hautamkosea mume wako siku sijazo. Na kama idadi ya wanaume uliyomwambia ni wengi anaweza kufikiri wewe ni kahaba au mzinzi.


Kwahiyo, iwapo atakuuliza ni wanaume wangapi ulishawahi kukutana nao kimwili, unaweza kucheka tu na umwambie: ''Ebu acha, tuanachane na hayo, lakini suala la ni wangapi halihusiani na safari ya mapenzi. ".

2. Kusema siri za mpenzi wako wa kiume au mume wako wakati mmoja

Ukiulizwa maswali kumuhusu mwanaume, mjibu machache

Usiseme mambo ambayo yanaweza kumfanya mume au mpenzi wako ahisi kwamba sio bora, au ajihisi kuwa mtu mbaya


Usizungumzie kuhusu -ungependa kuwa na uhusiano na mwanaume tajiri kiasi fulani, mwenye uwezo wa kingono kiasi gani, na ni kwa vipi ungependa ampende mke wake..

3. Usimwambie mume wako kwamba unampenda sana rafiki yako au shemeji yako
Sote tunafahamu kuwa inawezekana kwa rafiki au shemeji kutaka kukuoa.

Lakini, ni hatari kumwambia mume wako kuhusu wazo hili .

Sababu ni kwamba mume wako anaweza kuanza kuwa na mashaka kuhusu tabia zake na vitendo vyako kumuhusu mwanaume huyo, jambo linaloweza kusambaratisha ndoa yako.

4. Usijaribu kumwambia kuwa unamchukia mama yake au familia yake
Hata mama mkwe awe ni mtu mbaya kiasi gani, usimwambie mume wako kuwa unamchukia.


Au unaichukia familia yake. Hata kama umekasirika kiasi gani, usijaribu kusema mambo mabaya kuwahusu, au kumuona mume wako sawa na familia yake. .

Kama haupatani na yeyote katika familia ya mume wako, elezea kwa utulivu, ukiwa na matumaini kuwa ataelewa ni kwanini haupatani nao.

Mume wako pia ataweza kukusaidia kutatua tatizo, na pia itazuwia matatizo mengine ambayo yanaweza kusababisha matatizo makubwa zaidi.

5. Usimtishe mume wako kuwa utakuja kuachana naye

Siku utakapomwambia mume wako kuwa utaachana naye wakati mnazozana, jua ndio mwanzo wa malumbano ndani ya ndoa.

Ndoa itaanza kukumbwa na misukosuko, wasi wasi na kutoaminiana.

Kutishia kutoa talaka katika ndoa inamaanisha kuwa hauna moyo wa imani katika ndoa, na hauoni umuhimu wake.

Isipokuwa kama katika ndoa kuna unyanyasaji au uhalifu mwingine mbaya, ni vyema kujaribu kushirikiana kutatua changamoto zozote mlizonazo.




Download our APP from Google Playstore using the link here>>>

Join Our Telegram Channel for Daily Updates CLICK HERE

No comments:

Post a Comment

Edusportstz